Advertisements

Friday, February 8, 2019

MKUBWA NA WANAWE CREW WAANGUSHA SHANGWE LA KIBABE KWENYE TAMASHA LA SAUTI ZA BUSARA


Kundi la Mkubwa na Wanawe wakishambulia jukwaa katika onesho lao la jana usiku 7 Februari 2019, kwenye viunga vya Ngome Kongwe, Unguja, Zanzibar




NA ANDREW CHALE, ZANZIBAR

KUNDI la wanamuziki wanaokuzwa la Mkubwa na Wanawe usiku wa 7 Februari 2019  limeweza kukonga nyoyo za watu waliojitokeza kushuhudia tamasha la 16 la Kimataifa la Sauti za Busara, kwenye viunga vya Ngome Kongwe, Unguja.

Kundi hilo limeweza kuonesha umahri wao wa kuimba na kucheza jukwaani huku wakiendana sambamba na mapigo na ala za muziki wa bendi ‘live’, iliamsha shangwe za mara kwa  mara kwa mashabiki waliofurika Ngome Kongwe.

Vijana hao wa waliweza kuimba nyimbo zaidi ya tano (5)  ikiwemo ya Stata  ukiimbwa na mwanadada Catrima Wegesa  huku nyimbo zingine zikiimbwa na wasanii wengine Abdala Mustapha ‘Kisamaki’ huku kijana mdogo kabisa wa kundi hilo Abdul Kadry akiwa kivutio kila alipopanda kuimba kweney jukwaa hilo la Busara.

Dogo Kadry aliweza kuimba nyimbo zaidi ya mbili ikiwemo kuurudia wimbo wa Asu ulioimbwa na Abdul Misambano.
Aidha, Wasanii pia waliweza kuimba nyimbo za wasanii waliowahi kupitia kundi hilo zikiwemo za ‘Mototo wa udongo’  na ‘Watakubali’.

Kundi hilo lililo chini ya muasisi wake, Said Fella ‘Mkubwa Fella’ ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kilungule ya wilayani Temeke, Dar es Salaam hadi sasa lina vijana wanaofanya kazi za Sanaa za Muziki zaidi ya 100.

Miongoni wa wasanii waliowahi kuwa kwenye kundi hilo na kwa sasa wanajitegemea ni pamoja na Dogo Aslay, Mboso na wengine wengineo.

Miaka miaka kadhaa iliyopita wasanii hao Dogo Aslay na Mboso waliwahi kushiriki tamasha hilo huku wakiwa vijana wenye umri mdogo  ambapo walikuwa kivutio kama ilivyo kwa sasa  kwa msanii mpya wa kundi hilo Dogo Kadry.

Mpaka Mkubwa na Wanawake Crew wameshatoa nyimbo mbalimbali zikiwemo : Tofauti, 2012; Nawashusha Down, 2013; Fanya Yako, 2014; Unanitusi, 2015; Sitakitararira, 2016; Naelewa, 2016; Yerere, 2016

No comments: