Advertisements

Monday, February 11, 2019

MKUU WA MAJESHI YA ULINZI NA USALAMA VENANCE MABEYO AWASILI MKOANI NJOMBE KWA ZIARA YA SIKU MBILI

 Mwenyekiti wa Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania CDF, Venance Mabeyo, amewasili Mkoa wa Njombe na kupokelewa na  Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi Nchini Naibu Kamishna DCP Liberatus Sabas, katika ziara yake ya siku mbili mkoani humo kwa lengo la kujua nini chanzo cha matukio ya mauaji ya watoto yaliotokea siku za hivi karibuni. (Picha na Jeshi la Polisi).     
 Mwenyekiti wa Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania CDF Venance Mabeyo, akiteta jambo na Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi Nchini Naibu Kamishna DCP Liberatus Sabas, baada ya kuwasili katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe katika ziara yake ya siku mbili mkoani humo. (Picha na Jeshi la Polisi).    
Mwenyekiti wa Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Tanzania CDF Venance Mabeyo, akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama mkoani Njombe na kushoto kwake ni  Mkuu wa Operesheni Maalum za Jeshi la Polisi Nchini Naibu Kamishna DCP Liberatus Sabas. (Picha na Jeshi la Polisi).     

No comments: