Advertisements

Saturday, March 23, 2019

PROF. MBARAWA - NATAKA UFUATILIAJI NA KASI ZAIDI SEKTA YA MAJI

 Waziri wa Maji Prof. Makame Mbarawa (Mb) akiongea katika Baraza la Wafanyakazi la Wizara ya Maji jijini Dodoma. Waziri Mbarawa amewataka wafanyakazi kuongeza kasi, ubunifu na ufuatiliaji wa kazi mbalimbali katika sekta ya maji. Kulia ni Katibu Mkuu Prof. Kitila Mkumbo
 Katibu Mkuu Wizara ya Maji Prof. Kitila Mkumbo akiongea katika Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Maji. Prof. Kitila amesisitiza umuhimu wa ushirikishwaji wa Wafanyakazi katika mipango kwani wao ndio watekelezaji wakuu. Baraza hilo limefanyika katika ukumbi wa Wizara ya Maji jijini Dodoma.
Sehemu ya Wafanyakazi wa Wizara ya Maji waliohudhuria Baraza la Wafanyakazi wakiwasikiliza viongozi wa wizara wakati wa kikao cha Baraza kilichofanyika jijini Dodoma.

No comments: