Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda (kushoto) akimkaribisha Ubalozini Brig. Jenerali Chestino Msola, Kiongozi wa Ujumbe wa Washiriki wa Mafunzo kutoka Chuo cha Ulinzi cha Taifa (NDC) walipotembelea ubalozini hapo wakati wa ziara yao ya mafunzo ya siku tano nchini humo iliyoanza tarehe 10 Juni 2019.
Mhe. Balozi Luvanda (kushoto) akizungumza na Brid. Jenerali Msola (mwenye sare za jeshi za rangi ya kijani) pamoja na viongozi wengine wa ujumbe wa washiriki wa mafunzo kutoka Chuo cha Ulinzi cha Taifa (NDC) walipotembelea Ubalozi wa Tanzania nchini India wakati wa ziara yao ya mafunzo nchini humo. Kulia ni Comodore Michael Mumanga na Dkt. Lucy Shule, Mkurugenzi wa Mafunzo wa NDC.
Mhe. Balozi Luvanda akiendelea na mazungumzo na ujumbe huo kutoka NDC
Mhe. Balozi Luvanda akipokea zawadi ya ukumbusho (memento) kutoka kwa Brig. Jenerali Msola
Mhe. Balozi Luvanda akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa ujumbe wa washiriki wa mafunzo kutoka Chuo cha Ulinzi cha Taifa (NDC) walipotembelea Ubalozi wa Tanzania nchini India wakati wa ziara yao ya mafunzo nchini humo.
Mhe. Balozi Luvanda akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wote.







No comments:
Post a Comment