
Dar es Salaam. Makatibu wakuu wawili wa zamani wa CCM, Yusuf Makamba na Abdulrahman Kinana wamemwandikia barua katibu wa baraza la ushauri la viongozi wakuu wastaafu katika chama hicho, Pius Msekwa wakilalamika kudhalilishwa kwa mambo ya uzushi na uongo.
Lakini spika huyo wa zamani wa Bunge amewajibu, akiwashauri “wajibu mapigo”.
Mwenyekiti wa baraza hilo ni Rais Ali Hassan Mwinyi aliyeongoza Serikali ya Awamu ya Pili.
Makamba na Kinana, ambao walishika nafasi hizo kwa kufuatana wakati wa Serikali ya Awamu ya Nne, wamesema wametuma malalamiko yao “kwa kuzingatia katiba ya CCM, toleo la 2017 ibara ya 122”.
No comments:
Post a Comment