Advertisements

Thursday, July 18, 2019

MARAIS 16 KUKUTANA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA 39 WA SADC

Tanzania inatarajia kuwa mwenyeji na mwenyekiti wa mkutano wa 39 wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika SADC utakaofanyika Agosti, 2019 jijini Dar es salaam. Mkutano huo utatanguliwa na vikao vya awali kwaajili ya maandalizi na kutanguliwa na wiki ya maonesho ya bidhaa za ndani ujulikanao kama wiki ya viwanda ya SADC 22-26 Julai. Mkutano huo utahudhuriwa na viongozi wa nchi 16 zinazounda SADC. Mara ya mwisho Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano huo ilikuwa mwaka 2003 ambapo Rais Benjamini Mkapa alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa jumuiya hiyo.

No comments: