ANGALIA LIVE NEWS

Saturday, July 13, 2019

Msuguano wa Dk Kigwangala, Makamba nani amepotea njia?

By Faraja Kristomus, Mwananchi

Ukishakuwa mwanasiasa maarufu basi ni vema kufahamu kuwa kile unachokiandika kwenye mitandao ya kijamii kinaweza kukujenga au kukubomoa.

Mabishano kati ya mawaziri wawili, January Makamba na Dk Hamis Kigwangala kwenye mtandao wa Twitter hivi karibuni umetupa nafasi ya kuangalia mchango wa wafuasi wa wanasiasa na busara za viongozi tunaowachagua.

Kilichotokea
Mwandishi wa blogu kwa jina la Haki Ngowi alichapisha kwenye ukurasa wake wa Twitter kuhusu nia ya Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii kuanzisha mradi wa magari ya kupandisha watalii Mlima Kilimanjaro kupitia kwenye nyaya (cable cars). Baadaye Waziri January Makamba alimjibu Haki Ngowi kuwa hata kama hilo wazo la kuwa na mradi kama huo linaonekana kuwa zuri lakini bado ipo haja ya tathmini ya mazingira kufanyika kabla ya kuanza kuutekeleza.

Ndipo waziri mwenzake wa Maliasili na Utalii, Hamis Kigwangala alipoibuka na kumjibu January Makamba kuwa masuala ya tathmini za mazingira yanachelewesha maendeleo na yeye kama waziri analenga zaidi kuongeza mapato kupitia utalii. Akaenda mbali zaidi na kumshutumu mwenzake kuwa watu wa mazingira wanapenda sana makongamano. Kigwangala aliendelea kurusha mashambulizi ambayo hayawezi kuelezwa yote katika makala haya.

Baadaye Waziri Makamba akaona isiwe taabu, akaomba kutoendelea na malumbano na waziri mwenzake ambaye kwa hakika ameonyesha dhamira ya kuchapa kazi katika wizara yake na kuleta maendeleo. Hata hivyo, kauli ya Makamba haikumnyamazisha Kigwangala, aliendelea kumshambulia mwenzake. Hali hiyo iliwaibua mashabiki wa Makamba na kumshambulia Kigwangala kwa kumwita ni kiongozi aliyekosa busara.

No comments: