
By Charles Abel, Mwananchi
Kocha Mkuu wa Azam FC, Etienne Ndayiragije ameteuliwa kuwa Kocha Mkuu wa muda wa timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' kushika nafasi ya Emmanuel Amunike aliyetimuliwa.
Uteuzi wa Ndayiragije ambaye kwa sasa yuko nchini Rwanda akiiongoza Azam FC kwenye mashindano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kagame Cup) umetangazwa leo mara baada ya kamati ya utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kukutana kwa dharura jijini Dar es Salaam leo.
"Kikao hicho ambacho kipo kwa mujibu wa Katiba ya TFF Ibara ya 40 (110 kilifikia maamuzi hayo baada ya kujiridhisha na uwezo wa kocha huyo na mafanikio aliyoyapata, akifundisha timu mbakimbali za Tanzania ambazo ni Mbao na KMC. Ambapo Etienne akiwa na KMC katika msimu wake wa kwanza alifanikiwa kukiwezesha kikosi hicho kupata nafasi ya kucheza Kombe la Shirikisho la CAF pamoja na kutinga hatua ya nusu fainali ya Kombe la FA.
Kocha Mkuu wa Azam FC, Etienne Ndayiragije ameteuliwa kuwa Kocha Mkuu wa muda wa timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' kushika nafasi ya Emmanuel Amunike aliyetimuliwa.
Uteuzi wa Ndayiragije ambaye kwa sasa yuko nchini Rwanda akiiongoza Azam FC kwenye mashindano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kagame Cup) umetangazwa leo mara baada ya kamati ya utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kukutana kwa dharura jijini Dar es Salaam leo.
"Kikao hicho ambacho kipo kwa mujibu wa Katiba ya TFF Ibara ya 40 (110 kilifikia maamuzi hayo baada ya kujiridhisha na uwezo wa kocha huyo na mafanikio aliyoyapata, akifundisha timu mbakimbali za Tanzania ambazo ni Mbao na KMC. Ambapo Etienne akiwa na KMC katika msimu wake wa kwanza alifanikiwa kukiwezesha kikosi hicho kupata nafasi ya kucheza Kombe la Shirikisho la CAF pamoja na kutinga hatua ya nusu fainali ya Kombe la FA.
No comments:
Post a Comment