Advertisements

Wednesday, December 4, 2019

DKT. ABBASI AWAPIGA MSASA MAAFISA HABARI UANDAAJI WA TAARIFA KWA UMMA

Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi akiwasilisha mada kuhusu uandaaji wa taarifa kwa umma wakati wa mafunzo kwa Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali Jijini Dodoma leo tarehe 3 Desemba 2019. Mafunzo hayo yanafanyika ikiwa ni awamu ya pili kufanyika yameandaliwa kwa ushirikiano baina ya Idara ya Habari – MAELEZO na Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali (TAGCO). Majadiliano ya vikundi Baadhi ya Maafisa wakifanya mazoezi kwa vitendo ya namna ya uandishi wa Taarifa kwa Umma/Vyombo vya Habari wakati wa mafunzo ya Mawasiliano ya Kimkakati kwa Maafisa Habari kutoka wizara, taasisi, mashirika ya umma na halmashauri nchini leo tarehe 03 Desemba 2019 Jijini Dodoma. Mafunzo hayo yanafanyika ikiwa ni awamu ya pili kufanyika yameandaliwa kwa ushirikiano baina ya Idara ya Habari – MAELEZO na Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali (TAGCO). Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Wanyamapori Tanzania (TAWA), Bw. Twaha Twaibu akichangia mada wakati wa mafunzo ya Mawasiliano ya Kimkakati kwa Maafisa Habari kutoka wizara, taasisi, mashirika ya umma na halmashauri nchini leo tarehe 03 Desemba 2019 Jijini Dodoma. Mafunzo hayo yanafanyika ikiwa ni awamu ya pili kufanyika yameandaliwa kwa ushirikiano baina ya Idara ya Habari – MAELEZO na Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali (TAGCO). Mjumbe wa kamati tendaji ya Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali (TAGCO), Bw. Innocent Byarugaba akiwaongoza Maafisa Habari kumpongeza Mkurugenzi wa Idara ya Habari – MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi (mwenye suti nyeusi) mara baada ya kumaliza kuwasilisha mada kuhusu uandaaji wa taarifa kwa umma/vyombo vy habari wakati wa mafunzo ya Mawasiliano ya Kimkakati Maafisa hao leo tarehe 03 Desemba 2019 Jijini Dodoma.Kulia ni Katibu Mtendaji wa TAGCO, Bw. Abdul Njaidi. Mafunzo hayo yanafanyika ikiwa ni awamu ya pili kufanyika yameandaliwa kwa ushirikiano baina ya Idara ya Habari – MAELEZO na Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali (TAGCO). (Picha zote na: Idara ya Habari – MAELEZO)

No comments: