Advertisements

Thursday, December 5, 2019

WAZIRI SIMBACHAWENE AKUTANA NA MKUU WA SHIRIKA LA CHAKULA DUNIANI (WFP)

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mh. George Simbachawene akizungumza na Mkuu wa Shirika la Chakula Duniani (WFP) ambaye ni pia ni Kaimu Mkurugenzi Mkazi UN Nchini Tanzania, Bwana Michael Dunford, alipomtembelea Waziri katika Ofisi yake Luthuli jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mazungumzo kuhusiana na ushirikiano katika programu za Mazingira hususan mabadiliko ya tabia Nchi ambayo huathiri usalama wa chakula.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mh. George Simbachawene akifurahia jambo na Mkuu wa Shirika la Chakula Duniani (WFP) ambaye pia ni Kaimu Mkurugenzi Mkazi wa UN Nchini Tanzania, Bwana Michael Dunford alipomtembelea Ofisini kwake barabara ya Luthuli mapema hivi leo. Lengo la mazungumzo hayo ilikua ni kuhusu ushirikiano katika programu za Mazingira hususan mabadiliko ya tabianchi ambayo huathiri usalama wa chakula.

No comments: