Hii ni fursa nyingine muhimu kwa Tanzania kujitangaza na kuzidi kuvutia wadau zaidi katika Sekta ya Utalii, kuja kutembelea na kufanya biashara na Tanzania. Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi, Mhe. Irene F. M. Kasyanju tayari amekutana na wadau wote waliofika Uholanzi, kuhakikisha kuwa Tanzania inanufaika ipasavyo na maonesho hayo.
Maonesho hayo ambayo kwa lugha ya kidachi yanajulikana kama “Vakantiebeurs 2020” hufanyika mwezi Januari kila mwaka na yanahudhuriwa na mataifa mbalimbali duniani kwa lengo la kutangaza na kuuza vivutio vya Utalii na Burudani
Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi, Mhe. Irene Kasyanju (wa pili kushoto) akiwa na baadhi ya wawakilishi wa taasisi za Tanzania wanaoshiriki Maonesho ya Kimataifa ya Utalii nchini Uholanzi. Kutoka kushoto ni Bw. Michael Christian Makombe kutoka Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Bibi Alistidia Karaze kutoka Bodi ya Utalii Tanzania na Bw. Gerald Mono kutoka TANAPA.
Balozi Irene Kasyanju akipokea zawadi ya Kalenda za 2020 kutoka kwa Kiongozi wa ujumbe wa Tanzania kwenye Maonesho hayo, Bibi Alistidia Karaze ambaye ni Afisa Mkuu wa Utafiti na Maendeleo kutoka Bodi ya Utalii Tanzania (TTB).
Balozi Kasyanju akiwa na wawakilishi kutoka Hifadhi ya Ngorongoro, TTB, TANAPA; pamoja na Kampuni binafsi yaani, Nature’s Land Safaris & Rentals; na Mbalageti Safari zote kutoka Mwanza, Tanzania na Sea-cliff ya Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment