Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi aliyesimama akizindua Jukwaa la Haki Jinai Mkoa wa Singida. Kushoto ni Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP) Nchini, Biswalo Mganga na kulia in Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dkt. Angerina Lutambi
Baadhi ya watumishi wa Umma Singida walioshiriki kwenye uzinduzi wa Jukwaa la Haki Jinai Mkoa wa Singida( Picha Zote na John Mapepele,Singida
Picha ya pamoja baina ya Mkrugenzi wa Mashitaka,(DPP) Biswalo Mganga mwenye suti , Mkuu wa Mkoa wa Singida (mwwnye kilemba) anayefuata Dkt.Angelina Lutambi Katibu Tawala Mkoa wa Singida na wajumbe wa Jukwaa la Haki Jinai Mkoa wa Singida Mara baada ya kuzinduliwa kwa Jukwaa hilo la Mkoa
Na John Mapepele, Singida
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt. Rehema Nchimbi amezindua Jukwaa la Mkoa la Haki Jinai leo huku Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) Nchini, Biswalo Mganga akisema kuwa uzinduzi huu unafanywa kitaifa mkoani Singida na kuelekeza mikoa yote nchini kuzindua ili kusaidia kupambana na uhalifu wa kijina katika mikoa husika hivyo kupunguza mrundikano wa mahabusu.
Dkt. Nchimbi amesema kuzinduliwa kwa Jukwaa hili kutakuwa nguzo kuu ya kuzima uhalifu katika Mkoa wa Singida, huku akiwataka wajumbe kutumia jukwaa hili kufanya utatifi na kutafakari kwa kina ni namna gani bora ya kudhibiti uhalifu badala ya kusubili utokee na kupeleka kesi mahakamani, jambo ambalo amesema madhara yake yamekuwa makubwa.
“Namshukuru Mungu. Leo, kwangu ni siku ya kihistoria na ya kipekee ambayo nilitamani kuona inatimia tangu siku nyingi. Kila wakati nimekuwa nikiwasisitiza kuwa ni muhimu na ni lazima vyombo vyote vya Serikali katika mkoa wetu kufanya kazi ya kupambana na uhalifu kwa pamoja badala ya kila mmoja kujiona ni bora zaidi katika nafasi yake jambo halina tija na halitusaidii kama taifa, lakini hatimaye leo hili linatimia” alisisitiza



No comments:
Post a Comment