Advertisements

Friday, February 28, 2020

SAOHILL WAGAWA MICHE MILIONI MOJA KWA WANANCHI

Wananchi wakiendelea kuchukua miche ya miti kutoka Tarafa ya Nne ya Shamba la Miti SaoHill - Mgololo.
NA FREDY MGUNDA,SAO HILL.

ZAIDI ya miche milioni moja imegawiwa kwa wananchi wa vijiji vinavyolizunguka shamba la Miti SaoHill katika musimu wa mwaka wa 2019/2020 kwa lengo la kuimalisha ujirani mwema ambao umekuwa umedumu kwa miaka mingi.

Zoezi la ugawaji miche ya miti kwa ajili ya ujirani mwema hufanyika kila mwaka kipindi cha masika kwa lengo la kuhakikisha wanapanda miti hiyo na inakuwa kwa wakati,hasa kipindi hiki kizuri cha mvua za msimu.

Hatua ya ugawaji wa miche ya miti husaidia kwa kiasi kikubwa kuwakumbusha wananchi juu ya uhifadhi wa misitu katika maeneo yao kwani wanapochukua miche hiyo huelekezwa namna na ya kuipanda na tunzaji wake.

Hata hivyo wananchi wameendelea kuhimizwa juu ya utunzaji wa miti wanayoipanda ili iwe na manufaa kwao na vizazi vijavyo.

Shamba la Miti SaoHill ni miongoni mwa mashamba 23 ya miti ya kupandwa ya serikali yanayosimamiwa na Wakala wa Huduma wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) lenye ukubwa wa hekta 135,903 ambazo zimehifadhiwa kwaajili ya upandaji miti kibiashara na hifadhi ya mazingira na vyanzo vya maji,makazi ya watumishi na uwekezaji.

No comments: