Mke wa Mafumu amethibitishia kuwa mumewe amefariki, baada ya hali yake kubadilika ghafla.
Mafumu aliyejifinza kupiga Saxophone mwaka 1972 akiwa JKT Makutupora kwenye Brass Band yao, alikuwa akisumbuliwa na Kisukari kwa muda mrefu hali iliyopelekea kukatwa kwa mguu wake mmoja
Mkongwe huyo ameimba kwenye bendi ya African Stars ambayo hata jina lake alilibuni yeye na kutamba na vibao kama Sakatu Sakatu, Mayanga, Maya, Afrika na Dance Dance
Aidha, alitamba pia na bendi kadhaa zikiwemo Maquis, MK Group, Bicco Stars, Bima Lee, African Stars na African Beats
GPL

No comments:
Post a Comment