ANGALIA LIVE NEWS

Tuesday, May 12, 2020

Mwamuziki Mafumu Bilal Afariki Dunia

Mwanamuziki mkongwe wa muziki wa dansi nchini, Mafumu Bilal Bombenga maarufu ‘Super Sax’ amefariki Dunia Mei 11, 2020.

Mke wa Mafumu amethibitishia kuwa mumewe amefariki, baada ya hali yake kubadilika ghafla.

Mafumu aliyejifinza kupiga Saxophone mwaka 1972 akiwa JKT Makutupora kwenye Brass Band yao, alikuwa akisumbuliwa na Kisukari kwa muda mrefu hali iliyopelekea kukatwa kwa mguu wake mmoja

Mkongwe huyo ameimba kwenye bendi ya African Stars ambayo hata jina lake alilibuni yeye na kutamba na vibao kama Sakatu Sakatu, Mayanga, Maya, Afrika na Dance Dance

Aidha, alitamba pia na bendi kadhaa zikiwemo Maquis, MK Group, Bicco Stars, Bima Lee, African Stars na African Beats 
GPL

No comments: