Advertisements

Friday, March 29, 2024

RAIS DKT SAMIA KUONGOZA VIONGOZI WA SERIKALI KATIKA KUMBUKIZI MIAKA 40 YA HAYATI SOKOINE



Watanzania wote waalikwa katika ibada maalum ya kumbukizi ya miaka 40 Hayati Edward Moringe Sokoine,aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itakayofanyika Monduli juu mkoani Arusha Aprili 12,2024.

Taarifa hiyo imetolewa mapema leo hii Jijini Dodoma na Msemaji wa familia ya Hayati Sokoine Bwana Lembus Kipuyo alipokuwa akiongea na wanahabari, na kuongeza kuwa kumbukizi hii imeandaliwa na familia ikishirikiana na Taasisi ya hayat Edward Moringe Sokoine.

"Nawaalika watanzania wote kwenye ibada maalum ya kumbukizi ya miaka 40 ya Hayati Edward Moringe Sokoine, aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, itakayofanyika Ijumaa Aprili 12, 2024, katika Kijiji cha Enguik, Monduli Juu mkoani Arusha".

"Ibada hiyo itakayofanyika siku ya Ijumaa Aprili 12, 2024, saa 3:00 asubuhi, imeandaliwa na familia ikishirikiana na Taasisi ya Hayati Edward Moringe Sokoine".

Aidha Bwana Kipuyo amesema Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Dkt Samia Suluhu Hassan atawaongoza viongozi mbalimbali wa serikali katika kumbukizi hii.

"Ibada hiyo ya kumbukumbu ya Hayati Sokoine itawashirikisha viongozi mbalimbali wa Serikali wakiongozwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan".

Pia amezungumzia malengo ya kuanzishwa kwa Taasisi hiyo ya ya Hayati Edward Moringe Sokoine kuwa ni kuenzi mema aliyoyafanya katika Utumishi na enzi za uhai wake.

"Lengo kubwa la kuanzishwa kwa Taasisi ya Hayati Edward Moringe Sokoine, ni kuenzi mema aliyoyafanya, kwani aliacha alama kubwa ambayo taifa linamkumbuka hadi leo".

"Taasisi hiyo imejikita katika masuala ya elimu, kilimo, hifadhi ya mazingira, vyanzo vya maji pamoja na afya".

Sambamba na hayo yote hakuacha kuelezea uzalendo uliokuwa nao Hayati Edward Moringe Sokoine kwa taifa na wananchi kwa ujumla.

"Hayati Sokoine alikuwa mzalendo wa kweli, alipenda taifa lake na wananchi wake, alihakikisha kwamba rasilimali za nchi zinatumika na watanzania wote, aliwatumikia wananchi bila kubagua na alikuwa na hofu ya Mungu katika kufanya kazi zake".

"Hayati Sokoine alikuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika vipindi viwili wakati wa uongozi wa Awamu ya Kwanza. Alizaliwa Agosti 01, 1934, kijijini Enguik, Monduli Juu wilayani Monduli, mkoani Arusha".

No comments: