Tuesday, July 30, 2024

RAIS SAMIA AMTEUA CP. JEREMIAH KATUNGU KUWA MKUU WA JESHI LA MAGEREZA

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa Mkuu wa Jeshi la Magereza.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses M. Kusiluka, Kamishna wa Magereza CP. Jeremiah Yoram Katungu amepandishwa cheo kuwa Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) na kuteuliwa kuwa Mkuu wa Jeshi la Magereza.

CP Katungu anachukua nafasi ya CGP Mzee Ramadhani Nyamka ambaye amestaafu.
Uteuzi huu umeanza tarehe 28 Julai, 2024.

Sharifa B. Nyanga
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu

No comments: