Thursday, October 17, 2024

TCAA YASHIRIKI KONGAMANO LA PILI LA KIMATAIFA KATIKA SEKTA YA UCHUKUZI NA USAFIRISHAJI


Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa (kulia) akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Salim Msangi alipokuwa akitoa maelezo kuhusu mradi wa ujenzi wa Chuo cha Usafiri wa Anga (CATC) wakati wa Kongamano la pili la kimataifa katika sekta ya uchukuzi na usafirishaji, lilofanyika Oktoba 17, 2024, jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa akizungumza wakati wa kufungua kongamano la pili la kimataifa katika sekta ya uchukuzi na usafirishaji lililofanyika leo Oktoba 17, 2024, jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau kutoka sekta ya uchukuzi na usafirishaji wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Waziri wa Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa wakati wa ufunguzi wa kongamano la pili la kimataifa katika sekta ya uchukuzi na usafirishaji lililofanyika Oktoba 17, 2024, jijini Dar es Salaam.

REA YAPELEKA UMEME VITONGOJI 120 KIGOM



Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kutekeleza mradi wa kupeleka umeme kwenye majimbo 15 ya Mkoa wa Kigoma ambao utawezesha jumla ya vitongoji 120 kupata umeme wa uhakika utakaowarahisishia kufanya shughuli za kiuchumi na kujenga Taifa.

Hayo yemebainishwa leo Oktoba 16, 2024 na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Mhe. Thobias Andengenye mara baada ya kupokea taarifa ya REA kuhusu kuanza kwa utekelezaji wa miradi hiyo ya kupeleka umeme kwenye vitongoji 120 mkoani humo.

"Nawapongeza REA kwa kutekeleza mradi huu wa kupeleka umeme kwenye vitongoji. Umeme ni chachu ya maendeleo katika mkoa huu kwani unategemewa katika shughuli za kiuchumi na kijamii," Ameongeza Mhe. Andengenye.

Mhe. Andengenye ameitaka Kampuni ya Routeways Technologies Ltd inayotekeleza miradi hiyo kuhakikisha inaukamilisha mradi kwa wakati katika kipindi kilichopangwa katika makubaliano yao.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Miradi ya REA kanda ya Magharibi, Mha. Robert Dulle amesema wamemtambulisha mkandarasi huyo ambaye atatekeleza miradi ya vitongoji 15 kwa kila jimbo la uchaguzi katika mkoa wa Kigoma.

KATIBU MKUU LUHEMEJA AKIZUNGUMZIA BIASHARA YA KABONI

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mha. Cyprian Luhemeja amesema Kaboni sio biashara bali ni Utunzaji wa Mazingira wenye motisha kwa mtu ili aendelee kuhifadhi na kutunza mazingira.

Ameyasema hayo Oktoba 16, 2024 mkoani Morogoro alipotembelea Kituo cha Kitaifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC) ambapo ameeleza moja ya vitu ambavyo atahakikisha vinafanyika haraka ni katika kuwekeza kwenye kaboni.
Mh. Luhemeja amewataka wale wanaojihusisha na Kaboni kuongeza kasi katika utekelezaji wa maandiko ikiwa pamoja na kuwashawishi wengine waweze kujihusisha na utunzaji wa mazingira.

“Lengo la biashara ya kaboni ni katika kuhakikisha mazingira yanatunzwa yaani fedha inayopatikana inakusaidia kwenda kutunza eneo lingine la mazingira na kuyafanya maeneo mengi kuwa salama.”

Ameongeza ni vyema makampuni katika kuwekeza kwenye kaboni wakawa wengi ili kila mmoja aone faida yake itakayomshawishi naye kuingia katika utunzaji na uhifadhi wa mazingira ambapo baada ya miaka kadhaa nchi itakuwa salama zaidi kwenye mazingira.

MAKAMU WA PILI WA RAIS AZINDUA MITAMBO YA KUZALISHA GESI - HOSPITALI YA LUMUMBA


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akikata utepe kuashiria ufunguzi wa Mitambo ya uzalishaji wa Hewa Tiba(Oxygen Plants) uliofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mjini Magharibi - Lumumba….
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akizungumza na Viongozi wa Wizara ya Afya, wawakilishi kutoka mashirika mbali mbali, watendaji wa Wizara ya Afya na wananchi waliohudhuria katika ufunguzi wa Mitambo ya uzalishaji wa Hewa Tiba (Oxygen Plants) uliofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mjini Magharibi - LUMUMBA.


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla amesema Uwepo wa Mitambo ya uzalishaji wa Hewa Tiba (OXYGEN PLANTA) katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa Lumumba itaondoa kadhia na usumbufu wa utoaji wa huduma kwa wagonjwa katika hospitali zote za Serikali na Binafsi zilizopo hapa nchini.

Ameyasema hayo wakati wa uzinduzi wa Mitambo ya kuzalisha Hewa Tiba (Oxygen Plants) katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mjini Magharibi LUMUMBA,

OFISI YA MAKAMU WA RAIS YAWASILISHA TAARIFA KAMATI YA BUNGE


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akifafanua hoja mbalimbali wakati wa Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira kwa ajili ya kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Mkakati wa Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uchumi wa Buluu ya mwaka 2024 kwa kipindi cha Julai hadi Oktoba 2024 pamoja na taarifa ya utekelezaji wa Mkataba wa Nairobi wa Hifadhi ya Mazingira ya Bahari kilichofanyika Ofisi za Bunge jijini Dodoma Oktoba 16, 2024.

Serikali imesema itaendelea kusimamia na kuratibu kwa ufanisi shughuli za Uchumi wa Buluu nchini ili kuhakikisha wananchi inanufaika ipasavyo kwa kutumia rasilimali hizo kwa ukuaji wa uchumi na maendeleo endelevu.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji wakati wa Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira cha kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Mkakati wa Utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Uchumi wa Buluu ya mwaka 2024 kwa kipindi cha Julai hadi Oktoba 2024 pamoja na taarifa ya utekelezaji wa Mkataba wa Nairobi wa Hifadhi ya Mazingira ya Bahari jijini Dodoma Oktoba 16, 2024.

SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR, IMESEMA IMEPIGA HATUA KUBWA YA KUKABILIANA NA MAHITAJI YA MAKAZI YA WATU


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kuufungua Mkutano wa Mwaka wa Pamoja kati ya Umoja wa Afrika na Jumuiya za Taasisi Zinazojishughulisha na Mikopo ya Nyumba, mkutano huo unaofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Melia Kiwengwa Mkoa wa Kaskazini Unguja .
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kuufungua Mkutano wa Mwaka wa Pamoja kati ya Umoja wa Afrika na Jumuiya za Taasisi Zinazojishughulisha na Mikopo ya Nyumba, mkutano huo unaofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Melia Kiwengwa Mkoa wa Kaskazini Unguja.
WASHIRIKI wa Mkutano wa Mwaka wa Pamoja Kati ya Umoja wa Afrika na Jumuiya za Taasisi Zinazojishughulisha na Mikopo ya Nyumba, wakifuatilia hutuba ya ufunguzi wa mkutano huo, wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) akihutubia na kuufungua mkutano huo unaofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Melia Kiwengwa Mkoa wa Kaskazini Unguja.

WAZIRI MKUU AMWAKILISHA RAIS DKT SAMIA MAZIKO YA BABA WA KATIBU MKUU KIONGOZI

 
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa Oktoba 16, 2024 amemwakilisha Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika maziko ya Mzee Jeremiah Kusiluka ambaye ni Baba mzazi wa Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka yaliyofanyika katika kijiji cha Madihani, Makete mkoani Njombe.

Akitoa salamu za Mheshimiwa Rais Dkt. Samia, Waziri Mkuu amesema Mheshimiwa Rais Dkt. Samia ametoa wito kwa wanafamilia, ndugu na waombolezaji wawe watulivu katika kipindi hiki kigumu za msiba huo na waendelee kumuombea marehemu Mzee Jeremiah ili Mwenyezi Mungu amlaze mahali pema peponi.
Aidha, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa wanafamilia, ndugu na waombolezaji kuyaenzi mema yote aliyoyafanya marehemu kipindi cha uhai wake. “Tuenzi yale yote mema aliyoyafanya mzee wetu Jeremiah wakati wa uhai wake, tukifanya hivyo tutakuwa tumetenda haki.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema kuwa Makamu wa Rais Dkt. Philip Isdor Mpango na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Mwinyi wanatoa pole kwa wanafamilia, ndugu na waombolezaji kutokana na msiba huo.

Akizungumza kwa Niaba ya Familia, Prof. Lughano Kusiluka ametoa shukrani kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali kwa ujumla kwa kushiriki wake katika kumuaga Mzee Jeremiah. “Asanteni kwa kuja kushiriki nasi, tunawashukuru sana kwa kutuunga mkono kuja kushiriki nasi katika kumuaga mzee wetu, heshima hii ni kubwa na haielezeki. ”
Aliongeza kuwa Mzee Jeremiah alikuwa ni Baba imara na mwenye msimamo. “Mara zote alitusisitiza lazima tuheshimu watu tufanye kazi ili tuweze kuishi na alitukumbusha kuwa hapa katika kijiji cha Madihani, Kipahalo ni nyumbani kwetu. ” Alisema.

Kwa Upande wake Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka amesema kuwa Marehemu Mzee Jeremiah alikuwa ni mpenda maendeleo na watoto wake wote wamekuwa wakienzi msimamo huo. “Pamoja na kuwa mpenda maendeleo pia baba alikuwa mchaMungu na ameondoka akiwa mchaMungu.”

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI AJIANDIKISHA KWENYE DAFTARI LA MPIGA KURA


Na Mwandishi wetu- Dodoma
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Johari tarehe 16 Oktoba 2024 amejiandikisha, kwenye Daftari la Mpiga Kura katika Kata ya Ipagala Kituo cha Mbuyuni, Ilazo Jijini Dodoma ikiwa ni hatua kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 unaotarajia kufanyika Novemba 27 Mwaka huu.

Akizungumza mara baada ya kujiandikisha kwenye kituo hicho Mwanasheria Mkuu wa Serikali alitumia fursa hiyo kuwahamasisha Watumishi wote wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kujiandikisha katika Daftari la Mpiga Kura ili kutimiza haki yao ya msingi ya Kikatiba ya kupiga kura katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu.
“Nachukua nafasi hii kuwahamasisha Watumishi wote wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuhakikisha kwamba wanatumia haki yao vizuri ya kikatiba ya kupiga kura itakapofika tarehe 27 Novemba 2024 kwa ajili ya kuwachagua Viongozi wetu wa Serikali za Mitaa”.

Aidha, Mwanasheria Mkuu wa Serikali amewakumbusha Watumishi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kutimiza wajibu wa kujiandikisha kwenye Daftari la Mpiga Kura ili waweze kupata haki ya kushiriki kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

MRADI WA MAJI NGARA KUNUFAISHA MAELFU YA WANANCHI, HISTORIA NYINGINE KUANDIKWA

Na Mwandishi wetu - Fichuzi Blog.

Changamoto ya ukosefu wa maji safi na salama inatajwa kuwa historia kwa siku za usoni kwa wananchi wa Kijiji cha Katerere Kata ya kanazi Wilayani Ngara Mkoani Kagera baada ya Mbunge wa Jimbo hilo Mhe. Ndaisaba Ruhoro kukabidhi mradi wenye thamani ya shilingi Bilion 1.1 kwa Mkandarasi unaotekelezwa na serikali ya awamu ya sita Chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Makabidhiano hayo yamefanyika Oktoba 16, 2024 ambapo Mkandarasi anatarajiwa kuanza utekelezaji huo ndani ya siku saba ambao utatekelezwa kwa kipindi kisichozidi miezi nane ukiwa na lengo la Kumtua mama ndoo kichwani ambapo mara baada ya kukamilika wanatarajia kuingiza maji kwa kaya 100.
Mradi huo ambao ni neema kwa wananchi hao ni baada ya Serikali kufanya juhudi za muda mrefu za kuchimba visima ambavyo juhudi ziligonga mwamba kwa kukosa maji na hatimaye suluhisho limepatikana.

Ndaisaba amewataka wananchi kutunza mradi huo ili uweze kuwahudumia kwa muda mrefu ikiwa ni pamoja na kumtaka mkandarasi huyo kufanya kazi nzuri ili kutimiza mkakati wa Serikali ya kuhakikisha mwananchi anapata huduma zote muhimu kwa wakati.
Akizungumza kwa niaba ya wananchi Diwani wa Kata hiyo amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Mbunge wa Jimbo la Ngara kwa kufanikisha mpango wa wananchi kupata maji safi.

Wednesday, October 16, 2024

MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR- SIKU YA GANZI NA USINGIZI- DUNIANI- IDRISS ABDULWAKILI


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla akizungumza na Viongozi wa Wizara ya Afya, watendaji wa kada ya Ganzi na Usingizi, wanafunzi wa Afya na wananchi waliohudhuria katika Maadhimisho ya siku ya wataalamu wa Ganzi na Usingizi duniani yaliyofanyika katika Ukumbi wa Sheikh Idris Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Afya itaendelea kuhakikisha wataalamu wa ganzi na usingizi wanawekewa mazingira bora ya utendaji wa kazi zao ili kuendelea kufanyika upasuaji salama katika hospital zote nchini.

Hayo yamesemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla katika Maadhimisho ya siku ya wataalamu wa Gansi na Usingizi duniani yaliyofanyika katika Ukumbi wa Sheikh Idris Abdulwakil Kikwajuni Jijini Zanzibar.

Amesema Taaluma ya Ganzi na usingizi ni miongoni mwa Taaluma muhimu katika kada ya Afya hivyo Serikali itahakikisha inawawekea mazingira bora wataalmu hao ikowemo kuwapatia maslahi na stahiki zao zote pamoja na fursa za masomo ya ndani na nje ya nchi ili kuwaongezea ari ya utendaji wa kazi zao.

Mhe.Hemed amesema kuboreshwa na kuimarishwa kwa Sekta ya Afya nchini hususan katika kada ya Ganzi na Usingizi kutarejesha hadhi na heshima ya kada hio na kutawavutia vijana wengi zaidi kuipenda fani ya Ganzi na Usingizi ambao watasaidia kutoa huduma hio katika Hospitali mbali mbali nchini.

RAIS WA ZANZIBAR DKT. HUSSEIN MWINYI ATOA MKONO WA POLE KWA FAMILIA YA MAREHEMU TEREZA ALBAN ALI


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akisaini kitabu cha maombolezi cha Marehemu Tereza Alban Ali, aliyewahi kuwa Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, alipofika nyumbani kwa marehemu miembeni Wilaya ya Mjini Unguja 15-10-2024 na kutowa mkono wa pole kwa Familia ya marehemu.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amehudhuria msiba wa aliyewahi kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba, Marehemu Bi. Thereza Olban Ali nyumbani kwake Miembeni, Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi.
Dk. Mwinyi ametoa salamu za pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki.

Marehemu Bi. Thereza Olban alikua wanne kuzaliwa kwenye familia ya Shemasi Olban Ali na Bi. Christina Merry Ali, alizaliwa tarehe 15, Oktaba mwaka 1943 Mkunazini, Zanzibar.

BALOZI NCHIMBI: DEMOKRASIA NA HAKI ZA KIRAIA KUENDELEA KUIMARIKA CHINI YA RAIS SAMIA


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, ameithibitishia Jumuiya ya Kimataifa kuwa masuala ya demokrasia na haki za binadamu yataendelea kuimarika zaidi nchini Tanzania chini ya uongozi wa Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Balozi Nchimbi aliyasema hayo alipokutana na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Dr. Mehmet Güllüoğlu, Balozi wa Morocco, Mhe. Zacharia El Goumir, pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Sera na Tathmini wa Taasisi ya Misaada ya Marekani (MCC), kwa nyakati tofauti, leo Jumanne, tarehe 15 Oktoba 2024.
Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar es Salaam, Balozi Nchimbi amesema katika kipindi cha uongozi wa serikali ya awamu ya sita, hatua kubwa imefikiwa katika kuimarisha demokrasia, utawala bora, uchumi na haki za kiraia.

Mazungumzo hayo ya Balozi Nchimbi na mabalozi wa nchi hizo, pamoja na taasisi ya MCC, yalilenga kuboresha uhusiano katika nyanja mbalimbali, zikiwemo siasa, kilimo, teknolojia, elimu, na michezo, kwa lengo la kuleta maendeleo ya pamoja kwa wananchi wa pande zote.

PBZ YAFUNGUA TAWI LAKE MWANZA



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk, HusseinAli Mwinyi amesema kuwepo kwa Benki ya PBZ Tanzania Bara ni daraja muhimu la kuunganisha Muungano kwa Vitendo.

Rais Dk, Mwinyi hatua hiyo inaonesha ni jinsi Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inavyotoa Ushirikiano wa masuala ya kifedha kwa Zanzibar.
Rais Dk,Mwnyi ametoa tamko hilo leo tarehe 13 Oktoba alipozindua tawi la Bemki ya Watu wa ZanzibarPBZ, lilo Wilaya ya Nyamagana Mwanza.

Rais Dk, Mwinyi Amefahamisha kuwa PBz ni taasis ya kifedha inayomilikiwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ni Benki inayovutia Wananchi wengi kutokana na huduma zake na unafuu wa mikopo.

Amefahamisha kuwa kuendelea kufanya vizuri kwa Benki ya hiyo kunatokana na mtaji ilionao unaofikia Trilioni 2.3 na kuwa Benki inayofanya biashara ya zaidi ya Shilingi Trilioni moja na kuwa miongoni mwa Benki saba Bora hapa nchini.

MAKAMU WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR AFUNGUA JUKWAA LA UWEKEZAJI LA UTALII HALALI


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema Ujio wa Mufti Ismail Bin Mmussa Menk kutoka Nchini Zimbabwe umetoa fursa kwa Zanzibar kujitangaza zaidi kiutalii kupitia Utalii wa Maadili yani (HALAL TOURISM) uliojikita zaidi katika sheria na misingi ya Uislamu.

Ameyasema hayo katika hafla ya JUKWAA la UWEKEZAJI wa Utalii halali (HALAL TOURISM) lililofanyika katika Viwanja vya Hotel ya Verde Mtoni jijini Zanzibar.

Amesema uwepo wa Mufti Menki nchini umeitangaza Zanzibar kiutalii na kupata fursa ya kujifunza mambo mbali mbali kupitia Jukwaa la Utalii wa maadili lililotoa fursa kwa Mufti huyo na ujumbe wake aliokuja nao katika kuukumbusha umma umuhimu wa mikusanyiko ya dini na kuwa tayari kujitoa kwa ajili ya Allah.

Makamu wa Pili wa Rais amesema Serikali itaendelea kuboresha miundombinu mbali mbali ikiwemo ya barabara, Viwanja vya ndege na Bandari ambavyo vinachochea ukuwaji wa sekta ya Utalii nchini sambamba na kuviboresha vivutio vya utalii ili kuendelea kujitangaza kiutalii hasa katika maeneo ya kihistoria, kutangaza mila, silka na tamaduni njema zinazofuata mwenendo mzima wa kiislam ikiwemo Ibada, mavazi, ukarimu na ushirikiano katika jamii.

RAIS MHE. DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AKABIDHI TUZO KWA NSSF YA USIMAMIZI NA URATIBU WA HIFADHI YA JAMII KWA SEKTA BINAFSI NCHINI


Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) umeshinda tuzo ya Usimamizi na Uratibu wa Hifadhi ya Jamii kwa Sekta Binafsi nchini, wakati wa kilele cha Maonesho ya Saba ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yaliyofanyika kwenye uwanja wa EPZ Bombambili, mkoani Geita. Tuzo hiyo imetolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, na kupokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba wakati wa ufungaji wa maonesho hayo.
Aidha, NSSF imeshinda tuzo ya mshindi wa kwanza katika kundi la Hifadhi ya Jamii na Huduma za Bima zilizotolewa Oktoba 12, 2024 na Mhe. Anthony Mavunde, Waziri wa Madini, wakati wa maonesho hayo.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo, Bw. Mshomba amesema utoaji wa huduma kidijitali umekuwa nyenzo muhimu katika kuhakikisha huduma za NSSF zinawafikia wanachama popote walipo, ikiwemo kufungua madai ya kuomba mafao mbalimbali.

Tuesday, October 15, 2024

MWENDENDO WA UANDIKISHAJI JIJI LA DODOMA



Na. Faraja Mbise, DODOMA
Msimamizi wa Uchaguzi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko amekanusha taarifa zinazosambaa katika mitandao ya kijamii kuhusu mwenendo wa uandikishaji kuwa wanaandikishwa mamluki kwenye orodha ya wapiga kura.

Kanusho hilo alilitoa ofisini kwake alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kufuatia tuhuma zilizotolewa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kuhusu mwenendo wa uandikishaji orodha ya wapiga kura unaoendelea wakidai kuwa kituo kimoja kiliandikisha watu kinyume na utaratibu.
Dkt. Sagamiko alisema “kutokana na taarifa zilizosambaa katika mitandao ya kijamii, zinazoelezea kuhusu muenendo wa uandikishaji katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa bahati mbaya sana taarifa ile inaelezea kuhusu mwenendo mbaya wa uandikishaji.

Baada ya kupitia na kusikiliza kwa makini video ile, nikabaini kwamba tatizo sio mwenendo wa uandikishaji, bali tatizo ni uelewa mdogo juu ya kanuni na miongozo inayotumika katika uendeshaji wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu 2024”.

Monday, October 14, 2024

MARAFIKI WA GLORY NORTH CAROLINA WAMTOA OUT KWA CHAKULA CHA JIONI, GREENSBORO

Video marafiki wa Glory wakimuimbia wimbo wa kuzaliwa katika mgahawa wa Brazilian uliopo Greensboro, North Carolina siku ya Jumamosi Octoba 12, 2024 nchini Marekani
Glory akipuliza mshumaa huku marafiki zake wakimuangalia, kushoto ni Jane Hando na kati ni Flora Minja siku ya Jumamosi Octoba 12, 2024 Greensboro, North Carolina marafiki zake walipomtoa out kusherehekea siku ya kumbukizi ya siku ya kuzaliwa kwake.
Glory akijipongeza na kanywaji kidogo.
Glory akijipakulia minyama.
Picha juu na chini Glory akipata ukodak moment na marafiki zake
Glory na maraiki zake wakipata ukodak wa pamoja.
Kwa picha zaidi bofya soma zaidi

RAIS DKT. SAMIA ATETA NA ZUHURA YUNUS KILELE CHA MBIO ZA MWENGE

 
Rais wa  Jamuhuri ya Muungano Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiongea na Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Zuhura Yunus, jijini Mwanza leo  kwenye maadhimisho ya kilele cha mbio za Mwenge leo Oktoba 14,2024. Katikati ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Petrobas Katambi.

PICHA ZA MUONEKANO WA DARAJA LA JP. MAGUFULI LA KIGONGO - BUSISI


Muonekano wa Daraja la JP. Magufuli linalounganisha eneo la Kigongo (Misungwi) na Busisi (Sengerema) lenye urefu wa km 3 pamoja na barabara unganishi zenye urefu wa km 1.66 Mkoani Mwanza tarehe 13 Oktoba, 2024. Daraja hili litafunguliwa kwa matumizi Februari 2025.

KUKAMATWA KWA MWANAMKE KWA TUHUMA ZA MAUAJI ARUSHA


Na Mwandishi Jeshi la Polisi Arusha.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limesema linamshikilia Jaina Mchomvu kwa tukio la mauaji ya mtoto aitwaye Mariam Juma mwenye umri wa miaka 12 mkazi wa kwa Mrombo katika Halmashauri ya jiji la Arusha aliyekutwa ameauwa huku mwili wake ukiwa na majeraha ya kukatwa na kitu chenye ncha kali sehemu ya shingoni na maeneo mbalimbali ya mwili wake kisha mwili wake ukifichwa chini ya uvungu wa kitanda kwenye nyumba ya jirani yao.

Akitoa taarifa hiyo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Justine Masejo amesema awali mtoto huyu alikuwa ametumwa dukani toka asubuhi lakini hakurejea na ilipofika mchana wazazi wake walianza kumtafuta maeneo mbalimbali baada ya kuingiwa na wasiwasi.

SACP Masejo amesema hadi sasa tunawashikilia watu watatu akiwepo Jaina Mchomvu Mama mwenye nyumba ambaye amekamatwa na askari Polisi huko Mabogini Moshi, Mkoani Kilimanjaro alikokimbilia kujificha baada ya tukio hili kubaainika, mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mount Meru Arusha kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

BALOZI NCHIMBI ATOA SOMO UVCCM


-Awataka kushindana kwa hoja, akiwakabidhi jukumu zito Serikali za Mitaa

-Asema “CCM itawashinda kwa namna ambavyo hawajawahi kushindwa”

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, ametoa wito kwa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) pamoja na jumuiya nyingine za chama hicho kuendelea kushindana kwa hoja na kuwa mfano bora wanapojadili masuala mbalimbali ya kitaifa.

Akizungumza katika hafla ya kumaliza matembezi ya vijana kuadhimisha kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere, Balozi Nchimbi aliweka wazi kuwa nafasi ya CCM kushinda katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwezi Novemba inategemea sana juhudi za vijana hao.
Balozi Nchimbi, aliyekuwa akizungumza mbele ya vijana takriban 2,156 waliotembea kutoka Butiama, Mkoa wa Mara, hadi Nyamagana, Jijini Mwanza, alisisitiza umuhimu wa vijana wa CCM kuwa mstari wa mbele katika kutafuta kura kwa bidii.

Alieleza kuwa ushindi wa CCM hautapatikana kwa kubahatisha, bali kwa juhudi za makusudi na mipango ya kimkakati, huku akiwataka vijana hao kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha chama kinapata ushindi mkubwa.

RAIS SAMIA AZUNGUMZA NA WANANCHI WA SENGEREMA NA MISUNGWI MKOANI MWANZA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi mbalimbali pamoja na wananchi wa Sengerema mkoani Mwanza tarehe 13 Oktoba, 2024.
Shamrashamra za mapokezi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Sengerema mkoani Mwanza tarehe 13 Oktoba, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na mama mzazi wa mama Janeth Magufuli (Juliana Stephano Kidaso) mara baada ya kuwasili Kigongo Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza tarehe 13 Oktoba, 2024.