Tuesday, October 15, 2024

MWENDENDO WA UANDIKISHAJI JIJI LA DODOMA



Na. Faraja Mbise, DODOMA
Msimamizi wa Uchaguzi Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dkt. Frederick Sagamiko amekanusha taarifa zinazosambaa katika mitandao ya kijamii kuhusu mwenendo wa uandikishaji kuwa wanaandikishwa mamluki kwenye orodha ya wapiga kura.

Kanusho hilo alilitoa ofisini kwake alipokuwa akiongea na waandishi wa habari kufuatia tuhuma zilizotolewa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kuhusu mwenendo wa uandikishaji orodha ya wapiga kura unaoendelea wakidai kuwa kituo kimoja kiliandikisha watu kinyume na utaratibu.
Dkt. Sagamiko alisema “kutokana na taarifa zilizosambaa katika mitandao ya kijamii, zinazoelezea kuhusu muenendo wa uandikishaji katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa bahati mbaya sana taarifa ile inaelezea kuhusu mwenendo mbaya wa uandikishaji.

Baada ya kupitia na kusikiliza kwa makini video ile, nikabaini kwamba tatizo sio mwenendo wa uandikishaji, bali tatizo ni uelewa mdogo juu ya kanuni na miongozo inayotumika katika uendeshaji wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu 2024”.

Monday, October 14, 2024

MARAFIKI WA GLORY NORTH CAROLINA WAMTOA OUT KWA CHAKULA CHA JIONI, GREENSBORO

Video marafiki wa Glory wakimuimbia wimbo wa kuzaliwa katika mgahawa wa Brazilian uliopo Greensboro, North Carolina siku ya Jumamosi Octoba 12, 2024 nchini Marekani
Glory akipuliza mshumaa huku marafiki zake wakimuangalia, kushoto ni Jane Hando na kati ni Flora Minja siku ya Jumamosi Octoba 12, 2024 Greensboro, North Carolina marafiki zake walipomtoa out kusherehekea siku ya kumbukizi ya siku ya kuzaliwa kwake.
Glory akijipongeza na kanywaji kidogo.
Glory akijipakulia minyama.
Picha juu na chini Glory akipata ukodak moment na marafiki zake
Glory na maraiki zake wakipata ukodak wa pamoja.
Kwa picha zaidi bofya soma zaidi

RAIS DKT. SAMIA ATETA NA ZUHURA YUNUS KILELE CHA MBIO ZA MWENGE

 
Rais wa  Jamuhuri ya Muungano Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiongea na Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Zuhura Yunus, jijini Mwanza leo  kwenye maadhimisho ya kilele cha mbio za Mwenge leo Oktoba 14,2024. Katikati ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Petrobas Katambi.

PICHA ZA MUONEKANO WA DARAJA LA JP. MAGUFULI LA KIGONGO - BUSISI


Muonekano wa Daraja la JP. Magufuli linalounganisha eneo la Kigongo (Misungwi) na Busisi (Sengerema) lenye urefu wa km 3 pamoja na barabara unganishi zenye urefu wa km 1.66 Mkoani Mwanza tarehe 13 Oktoba, 2024. Daraja hili litafunguliwa kwa matumizi Februari 2025.

KUKAMATWA KWA MWANAMKE KWA TUHUMA ZA MAUAJI ARUSHA


Na Mwandishi Jeshi la Polisi Arusha.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limesema linamshikilia Jaina Mchomvu kwa tukio la mauaji ya mtoto aitwaye Mariam Juma mwenye umri wa miaka 12 mkazi wa kwa Mrombo katika Halmashauri ya jiji la Arusha aliyekutwa ameauwa huku mwili wake ukiwa na majeraha ya kukatwa na kitu chenye ncha kali sehemu ya shingoni na maeneo mbalimbali ya mwili wake kisha mwili wake ukifichwa chini ya uvungu wa kitanda kwenye nyumba ya jirani yao.

Akitoa taarifa hiyo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Justine Masejo amesema awali mtoto huyu alikuwa ametumwa dukani toka asubuhi lakini hakurejea na ilipofika mchana wazazi wake walianza kumtafuta maeneo mbalimbali baada ya kuingiwa na wasiwasi.

SACP Masejo amesema hadi sasa tunawashikilia watu watatu akiwepo Jaina Mchomvu Mama mwenye nyumba ambaye amekamatwa na askari Polisi huko Mabogini Moshi, Mkoani Kilimanjaro alikokimbilia kujificha baada ya tukio hili kubaainika, mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mount Meru Arusha kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

BALOZI NCHIMBI ATOA SOMO UVCCM


-Awataka kushindana kwa hoja, akiwakabidhi jukumu zito Serikali za Mitaa

-Asema “CCM itawashinda kwa namna ambavyo hawajawahi kushindwa”

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, ametoa wito kwa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) pamoja na jumuiya nyingine za chama hicho kuendelea kushindana kwa hoja na kuwa mfano bora wanapojadili masuala mbalimbali ya kitaifa.

Akizungumza katika hafla ya kumaliza matembezi ya vijana kuadhimisha kumbukumbu ya Mwalimu Julius Nyerere, Balozi Nchimbi aliweka wazi kuwa nafasi ya CCM kushinda katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwezi Novemba inategemea sana juhudi za vijana hao.
Balozi Nchimbi, aliyekuwa akizungumza mbele ya vijana takriban 2,156 waliotembea kutoka Butiama, Mkoa wa Mara, hadi Nyamagana, Jijini Mwanza, alisisitiza umuhimu wa vijana wa CCM kuwa mstari wa mbele katika kutafuta kura kwa bidii.

Alieleza kuwa ushindi wa CCM hautapatikana kwa kubahatisha, bali kwa juhudi za makusudi na mipango ya kimkakati, huku akiwataka vijana hao kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha chama kinapata ushindi mkubwa.

RAIS SAMIA AZUNGUMZA NA WANANCHI WA SENGEREMA NA MISUNGWI MKOANI MWANZA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi mbalimbali pamoja na wananchi wa Sengerema mkoani Mwanza tarehe 13 Oktoba, 2024.
Shamrashamra za mapokezi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Sengerema mkoani Mwanza tarehe 13 Oktoba, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na mama mzazi wa mama Janeth Magufuli (Juliana Stephano Kidaso) mara baada ya kuwasili Kigongo Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza tarehe 13 Oktoba, 2024.

TAA YAWAFIKIA WADAU WA UTALII KATIKA MAONESHO YA S!TE

 

Maonesho ya Swahili International Tourism Expo (S!TE) mwaka 2024 yamehitimishwa rasmi jijini Dar es Salaam, yakiteka hisia za wengi kwa mafanikio makubwa ya kuingiza takribani wanunuzi 120 wa kimataifa wa bidhaa za utalii. 
Katika hafla ya kufunga maonesho hayo kwenye ukumbi wa Mlimani City, Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Dkt. Pindi Chana, alieleza kuwa mwitikio wa washiriki umeongezeka, akitaja filamu maarufu ya "The Royal Tour" aliyotengeneza Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kama kichocheo muhimu.

"Utalii unachangia kwa kiasi kikubwa pato la taifa, kuanzia pale mtalii anaposhuka uwanja wa ndege, hadi anapohudumiwa na hoteli na kufanya shughuli mbalimbali," alisema Dkt. Chana.

Pia katika maonesho hayo Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) iliweza kutoa elimu kwa wananchi mbalimbali pamoja na kupoke mapendekezo au changamoto wanazozipitia wakati wa kutumia miundombinu ya Mamlaka hiyo.
Afisa Masoko kutoka TAA Shaaban Towo akitoa maelezo kwa Mkuu wa Kitengo cha Undeshaji Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Terminal 3 Keneth Lwejuna aliyetembelea Banda la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kwenye maonesho ya Nane ya Swahili International Tourism Expo (S!TE 2024) katika Ukumbi wa Mlimani City mkoani Dar es Salaam.
Afisa Uhusiano Mwandamizi kutoka TAA Mariam Lussewa akitoa maelezo kuhusu Mamlaka hiyo pamoja na kusikiliza changamoto mbalimbali kwa mwananchi aliyetembelea banda la Mamlaka hiyo kuhusu kazi zinazofanywa na Mamlaka hiyo wakati wa maonesho ya Nane ya Swahili International Tourism Expo (S!TE 2024) katika Ukumbi wa Mlimani City mkoani Dar es Salaam.

Sunday, October 13, 2024

RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AFUNGA MAONESHO YA SABA YA TEKNOLOJIA NA UWEKEZAJI KWENYE SEKTA YA MADINI KITAIFA MKOANI GEITA



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiangalia mfano wa uchimbaji mdogo wa madini ya dhahabu wakati wa Maonesho ya Saba ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye sekta ya madini yaliofanyika Mkoani Geita tarehe 13 Oktoba, 2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na watoto wakati alipopita kukagua mabanda mbalimbali ya Maonesho ya Saba ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye sekta ya madini yaliofanyika Mkoani Geita tarehe 13 Oktoba, 2024.

MHE OTHMAN AKUTANA NA UJUMBE WA BODI YA WAKURUGENZI YA BARAZA LA TAIFA LA HIFADHI NA USIMAMIZI WA MAZINGIRA (NEMC)


Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amesema kwamba Zanzibar inatatizo kubwa la uharibifu wa mazingira linalohitaji jitihada za pamoja kati ya wadau, wahisani na washirika mbali mbali ili kuweza kulikabili ipasavyo na kupunguza athari zitokanazo na changamoto hiyo.

Mhe. Othman ameyasema hayo huko nyumbani kwake Chukwani Zanzibar alipofanya mazungunzo na Ujumbe kutoka Bodi ya Wakurugenzi ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), ulioongozwa na Mwenyekiti wake Profesa Esnati Osinde Chaggu.

Mhe. Othman amesema kwamba changamoto hiyo inayotokana na athari za mabadiliko ya tabia nchi ni vita kubwa ya kimazingira na ni jambo ambalo haliwezi kushughulikiwa ipasavyo pasipo jitihada za pamoja kati ya wadau, wahisani pamoja na wataalamu sambamba na kupatikana rasilimali za aina mbali mbali.
Amefahamisha kwamba maeneo mengi yameharibika na kwamba ni vigumu kwa Zanzibar pekee kwa nguvu za waliopewa dhamana ya usimamizi wa mazingira kuweza kuyarejeshea hali yake ya uasili pasipo na jitihada za pamoja kutoka ndani na nje ya nchi.

Mhe. Othman ameutaka uongozi wa Bodi hiyo kuhakikisha wanalichukua suala la changamoto ya uharibifu wa mazingira kwamba ni la wote hasa kwavile katika mtazamo wa kimataifa Tanzania ndio mlango wa wakutambuliwa.

UFUNGUZI WA KONGAMANO LA KWANZA LA KIMATAIFA LA LIGHT UPON LIGHT ZANZIBAR


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Mufti Mkuu wa Zimbabwe Sheikh Ismail Menk, alipowasili katika Uwanja wa New Amaan Complex Zanzibar kwa ajili ya ufunguzi wa Kongamano la Kwanza la Kimataifa la Light Upon Light Zanzibar, lililofanyika 12-10-2024 katika uwanja huo.(Picha na Ikulu)

WASHIRIKI wa Kongamano la Kwanza la Kimataifa la Light Upon Light Zanzibar, wakifuatilia kongamano hilo lililofanyika katika Uwanja wa New Amaan Complex Zanzibar, wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi, (hayupo pichani) akihutubia na kulifungua kongamanbo hilo lililofanyika  12-10-2024 na kuwashirikisha Masheikh na Wanavyuoni mbalimbali na Mufti Mkuu wa Zimbabwe Sheikh.Ismail Menk .(Picha na Ikulu)

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwasili katika Uwanja wa New Amaan Complex Zanzibar, akielekea katika jukwaa maalumu kwa ajili ya Ufunguzi wa Kongamano la Kwanza la Kimataifa la Light Upon Light Zanzibar , lililofanyika 12-10-2024 na (kulia kwa Rais) Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Alhajj Hemed Suleiman Abdulla na (kushoto kwa Rais) Waziri wa Nchi Afisi ya Rais, Katiba,Sheria,Utumishi na Utawala Bora Zanzibar Alhajj Haroun Ali Suleiman.(Picha na Ikulu)
/RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk.Hussein Ali Mwinyi akihutubia na kulifungua Kongamano la Kwanza la Kimataifa la Light Upon Light Zanzibar, lililofanyika katika Uwanja wa New Amaan Complex Zanzibar jana 12-10-2024.(Picha na Ikulu)

MAZRUI AHIMIZA KUSOMEA KADA YA GANZI NA USINGIZI


Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui amewashauri vijana wanaosomea kada ya afya kutumia fursa ya kusomea kada ya ganzi na usingizi ili kukidhi hitaji la nchi kwa wataalam wa kada hiyo ambao kwa sasa wapo wachache.

Ushauri huo aliutoa na alipozungumza na waandishi wa habari kuelekea siku ya wataalamu wa ganzi na usingizi duniani ambapo amesema Zanzibar bado inakabiliwa na uhaba wa wataalamu hao.
Amesema Kada ya Ganzi na Usingizi bado inahitaji wataalamu kutokana na umuhimu wake katika sekta ya afya nchini na serikali ya mapinduzi Zanzibar imejidhatiti kuwasomesha wataalamu hao na kuwawekea mazingira mazuri pamoja na maslahi yao.
Hata hivyo Waziri Mazrui amesema kuwa milango ya wizara ipo wazi kuwapa ushauri vijana wanaotaka kujiendeleza katika taaluma ili waweze kuchagua kada hiyo ya ganzi na usingizi.
Amefahamisha kuwa Zanzibar ina wataalamu bingwa wa ganzi na usingizi wanne wataalamu wa ngazi ya shahada ya kwanza 2 na ngazi nyengine 18 Unguja na Pemba ambao wanatengeneza idadi ya wataalamu 49.

Saturday, October 12, 2024

JUKWAA LA WANAWAKE KATIKA USAFIRI WA ANGA LATEMBELEA KITUO CHA WATOTO YATIMA CHA ROLINA


Katika kuadhimisha siku ya mtoto wa Kike Duniani, Jukwaa la Wanawake katika Usafiri wa Anga Tanzania (WIA-TZ) kwa kushirikiana na Jukwaa la Viongozi katika usafiri wa Anga Afrika (Afican Leaders in Aviation-ALA) wametembelea kituo cha kulelea watoto yatima cha Rolina kilichopo Kwa Sadala mkoani Kilimanjaro na kutoa elimu na uelewa wa sekta ya Usafiri wa Anga.
Akizungumza katika ziara hiyo, Khodana Davhana Mwanzilishi mwenza wa Jukwaa la Viongozi katika Usafiri wa Anga barani Afrika, ameeleza kuwa wanatembelea nchi mbalimbali barani Afrika hususani katika shule na vituo kwa lengo la kuhamasisha vijana hasa wa kike kujiunga na sekta ya usafiri wa anga.
Amesisitiza kuwa masomo yoyote ikiwemo sheria, biashara, udaktari, sayansi n.k yatamuwezesha kijana wa kike kujiunga na sekta ya anga.

Wanachama wa WAI – TZ Bi Upendo Mwaibale Afisa mtoa taarifa za anga na Bi Fatma Kawale, Afisa Uongozaji Ndege walitoa elimu ya usafiri wa Anga na kuwahimiza vijana hasa watoto wa kike kuchukua masomo ya Sayansi, Teknolojia, Hesabu na Uhandisi ili waweze kuingia katika sekta ya Usafiri wa anga, lakini pia waliwahimiza kuishi ndoto zao ili kufikia malengo yao.

IMF NA BENKI YA DUNIA ZAITEUA TANZANIA KUNUFAIKA NA MPANGO WA KUKABILIANA NA ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI


Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akiongoza kikao cha Wataalam kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na Benki ya Dunia, kilichofanyika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, Jijini Dar es Salaam, ambapo ilitolewa taarifa kuwa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na Benki ya Dunia (World Bank Group), zimeitangaza Tanzania kuwa nchi ya pili, baada ya Madagascar, kunufaika na Mfumo wa Ushirikiano wa Kuimarisha Hali ya Hewa kwa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na athari mbaya za uharibifu wa mazingira.
 
Ujumbe kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) ukiongozwa na Kiongozi wa Timu ya Wataalam kutoka Shirika hilo, Bw. Charalambos Tsangarides (kulia), ukiwa katika kikao na Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), kilichofanyika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha, Jijini Dar es Salaam, ambapo ilitolewa taarifa kuwa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) na Benki ya Dunia (World Bank Group), zimeitangaza Tanzania kuwa nchi ya pili, baada ya Madagascar, kunufaika na Mfumo wa Ushirikiano wa Kuimarisha Hali ya Hewa kwa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na athari mbaya za uharibifu wa mazingira.

MAKAMU WA RAIS AJIANDIKISHA DAFTARI LA WAPIGA KURA BUHIGWE







Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango na Mwenza wake Mama Mbonimpaye Mpango wameshiriki zoezi la Uandikishaji kwenye Daftari la Wapiga kura kwaajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika Kitongoji cha Kihanga Kijiji cha Kasumo Wilaya ya Buhigwe Mkoani Kigoma. Tarehe 12 Oktoba 2024.

RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN AWASILI MKOANI MWANZA KWA AJILI YA KUHITIMISHA KILELE CHA MBIO ZA MWENGE WA UHURU PAMOJA NA WIKI YA VIJANA




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na viongozi mbalimbali mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza tarehe 12 Oktoba, 2024.