Tuesday, October 29, 2013

MAREKANI YATETEA MSIMAMO WAKE WA KUIWEKEA CUBA VIKWAZO VYA KIUCHUMI

Muwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi akizungumza wakati wa upigaji kura wa Azimio nambari A/68/L4 linaloitaka Marekani kuiondolea Cuba Vikwazo vya Kiuchumi, Kibiashara na Kifedha. Pembeni ni Naibu Muwakilishi wa Kudumu, Balozi Ramadhan Mwinyi. Nchi 188 kati ya nchi 194 ambazo ni Mwanachama wa Umoja wa Mataifa zilipiga kura ya ndiyo kuunga mkono azimio hilo katika mkutano uliofanyika siku ya Jumanne hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa zikiwamo nchi zote za Jumuiya ya Ulaya ilihali Marekani na Israel zilipiga kura ya hapana huku nchi tatu ambazo ni Marshall Island, Micronesia na Palau zilipiga kura ya kutofungamana na upande wowote.

No comments: