Advertisements

Tuesday, August 1, 2017

EWURA yatangaza bei mpya ya mafuta, Petroli, Dizeli bei zashuka

Mamlaka ya Udhibiti wa huduma za Nishati na Maji (EWURA) imetangaza bei mpya za mafuta ambazo zinaanza kutumika kesho ambapo bei ya mafuta ya Petroli imeshuka kwa shilingi 36 kwa lita, Dizeli ikishuka kwa shilingi 44 kwa lita, ilihali bei ya mafuta ya taa ikipanda kwa shilingi 24 kwa lita.
Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Mamlaka hiyo, Titus Kaguo amesema bei hizo ni kwa mafuta yanayopakuliwa jijini Dar es Salaam, ili hali yale ya mkoani tanga yakibakia bei yake ileile ya mwezi uliopita.

No comments: