Friday, September 8, 2017

Serikali yaombwa kutoa kipaumbele upatikanaji mikopo nafuu ya kilimo

Afisa Utafiti na Uchambuzi wa TGNP, Maureen Mbolene akitoa maelekezo kwa washiriki wa washa hiyo.
Mwakilishi wa Forum CC, Jackson Massawe (aliye simama) akiwasilisha mada kwa wakulima, wachimbaji wadogowadogo na wanaharakati ngazi ya jamii wanaoshiriki katika Tamasha la Jinsia Tanzania 2017.
Sehemu ya wakulima, wachimbaji wadogowadogo na wanaharakati ngazi ya jamii wanaoshiriki katika Tamasha la Jinsia Tanzania 2017 wakifuatilia mada anuai toka kwa wawasilishaji. 
Sehemu ya wakulima, wachimbaji wadogowadogo na wanaharakati ngazi ya jamii wanaoshiriki katika Tamasha la Jinsia Tanzania 2017 wakifuatilia mada anuai toka kwa wawasilishaji.

SERIKALI imeobwa kutoa kipaumbele katika upatikanaji wa mikopo nafuu ya kilimo kwa wanawake, ikiwa ni pamoja na kupewa haki ya kupata na kumiliki mashamba ili kuongeza tija katika uzalishaji wa bidhaa za kilimo.

Kauli hiyo imetolewa na Mwakilishi wa Forum CC, Jackson Massawe alipokuwa akiwasilisha mada kwa baadhi ya wakulima, wachimbaji wadogowadogo na wanaharakati ngazi ya jamii wanaoshiriki katika Tamasha la Jinsia Tanzania 2017 linaloendelea katika viwanja vya TGNP Mabibo Dar es Salaam.

Alisema Sekta ya Kilimo nchini Tanzania imebebwa na wanawake, na wao ni uti wa mgongo katika nguvukazi ya kilimo Tanzania. Aliongeza kuwa wanawake wanaoshiriki katika sekta ya kilimo ni takribani asilimia 70 kiwango ambacho ni kikubwa ukilinganisha na wanaume.

Bw. Massawe aliishauri Serikali kuongeza bajeti katika sekta ya kilimo huku ikiwa na mrengo wa kijinsia, huku ugawaji wa fedha za bajeti ufanyike kama ilivyokusudiwa.

Naye, Mwakilishi kutoka Taasisi ya Ekama, Lucia Akaro akiwasilisha mada ya Ukatili wa jinsia kwenye kilimo alisema bado idadi kubwa ya wanawake wamekuwa wakikabiliwa na vitendo hivyo katika gazi za familia.

Alisema kuna kila sababu vitengo husika kutoa elimu kwa jamii kuhusu athari za ukatili wa jinsia, hasa kwa kundi la wanaume katika mapambano ya kuhakikisha ukatili wa jinsia unapingwa vikali na makundi yote.

"...Wanawake wengi hukumbana na ukatili wa jinsia ambao unasababishwa mara nyingi na wanaume kuanzia ngazi ya familia ikiwa ni pamoja na kumnyima mwanamke uhuru wa kufanya maamuzi katika ngazi ya familia hususani kwenye kipato cha familia. Hii husababishwa na miiko na majukumu ya kijinsia na kutokuwa na nguvu sawa kati ya mwanaume na mwanamke.,"

Aidha alizitaja changamoto zingine zinazowakabili wakulima ni pamoja na mvua zisizo za uhakika, kupotea kwa vyanzo vya maji na mlipuko wa magonjwa kwa mimea na mifugo kama vile kanitangaze na mnyauko.

Aliitaka Serikali pia kukabiliana na changamoto zinazotokana na mabadiliko ya tabia nchi, kundi la wanawake ndilo linaloathika zaidi na mabadiliko ya Tabianch

No comments: