Advertisements

Wednesday, October 11, 2017

WAFANYAKAZI WA BENKI YA NMB,MATAWI YA MAWENZI NA MBUYUNI MJINI MOSHI WAFANYA USAFI NA KUTOA ZAWADI KWA WAGONJWA ,HOSPITALI YA ST JOSEPH.

Wafanyakazi wa Benki ya NMB ,Matawi ya Mawenzi na Mbuyuni wakiwa katika Hospitali ya St,Joseph mjini Moshi kwa ajili ya zoezi la usafi pamoja na kutoa zawadi kwa wagonjwa waliolazwa katika hospitali hiyo ikiwa ni muendelezo a wiki ya huduma kwa wateja.
Mmoja wa watumishi wa Hosptali ya St Joseph akimvisha kizuia vumbi ,mfanyakazi wa Benki ya NMB walipofika hospitalini hapo kwa ajili ya kufanya usafi.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya St Joseph Sista,Ubanus Lyimo akimvisha kofia maalumu Menenja wa Benki ya NMB,tawi la Mawenzi kabla ya kuanza zoezi la Usafi katika Hospitali hiyo.
Wafanyakazi wa Benki ya NMB,matawi ya Maeenzi na Mbuyuni mjini Moshi wakishiriki zoezi la usafi eneo la nje ya Hospitali ya St Joseph ikiwa ni sehemu ya kuendelea na maadhimisho ya wiki ya huduma kwa watena.
Wafanyakazi wa Benki ya NMB wakichoma moto taka mara baada ya kuhitimisha zoezi la usafi katika Hospitali hiyo
Wafanyakazi wa NMB,matawi ya Mawenzi na Mbuyuni mjini Moshi ,wakiwa wameshikilia Fagio mara baada ya kuhitimisha zoezi la usafi katika Hospitali ya St Joseph.
Afisa Mikopo katika Benki ya NMB,tawi la Mawenzi mjini Moshi,Elikana Boyi akikabidhi mche wa sabani kwa mmoja wa wagonjwa waliolazwa katika hospitali ya St Joseph Mjini Moshi.
Meneja wa NMB,tawi la Mawenzi ,Johnson Urasa akiweka mche wa sababuni mbele ya mtoto aliyelazwa katika hospitali ya St Joseph ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya huduma kwa wateja.
Meneja wa Benki ya NMB,tawi la Mbuyuni ,Rose Manyoni (katikati) akisaidiana na mwenzake kumuinua mmoja wa wagonjwa waliolazwa katika Hospitali ya St Joseph walipofika kuwajulia hali pamoja na kutoa zawadi. 
Mganga Mkuu wa Hospitali ya St Joseph ya mjini Moshi,Sista Ubanus Lyimo akizungumza mara baada ya Wafanyakazi wa Benki ya NMB,matawi ya Mawenzi na Mbuyuni kuhitimisha zoezi la kutoa zawadi kwa wagonjwa waliolazwakatika hospitali hiyo.
Meneja wa Benki ya NMB,tawi la Mawenzi ,Johnson Urasa akizungumza mara baada ya kuhitimisha zoezi la kufanya usafi pamoja na utoaji wa zawadi kwa wagonjwa waliolazwa katika Hospitali hiyo.
Wafanyakazi wa Benki ya NMB,matawi ya Mawenzi na Mbuyuni wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuhitimisha zoezi la kufanya usafi na utoaji wa zawadi kwa wagonjwa waliolazwakatika Hospitali ya St Joseph ya mjini Moshi.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini.

No comments: