Advertisements

Friday, February 16, 2018

MAFUNZO YA UONGOZI KWA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI YAFANYIKA JIJINI DAR

 Afisa Mkuu wa Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika kutoka Manispaa ya Kinondoni,Saleh Hijja Mohamed (aliyesimama) akizungumza kabla ya kumalizika kwa semina ya siku tatu ya mafunzo ya uongozi kwa walimu wa shule za msingi na sekondari wa Jiji la Dar es Salaam leo. Semina hiyo imefanyika katika Kituo cha Walimu cha Mzimuni kilichopo Magomeni Mapipa. Kulia wanaoshuhudia ni Afisa Mkuu wa Miradi wa Shirika lisilo la Kiserikali la British Council,Atiya Sumar na Meneja Miradi wa Shirika hilo,Ephraim Kapungu. Picha na Elisa Shunda
 Afisa Mkuu wa Miradi wa Shirika lisilo la Kiserikali la British Council, Atiya Sumar akizungumza katika ufungaji wa semina hiyo.
 Meneja Miradi wa Shirika Lisilo la Kiserikali la British Council, Ephraim Kapungu (katikati) akielezea utendaji kazi wa shirika hilo katika uwezeshaji wa masuala mbalimbali yahusuyo elimu jinsi shirika hilo linavyofanya kazi zake kwa kushirikiana na serikali kupitia wizara ya elimu.
 Mmoja kati ya wakufunzi wa semina hiyo Ndg.Edwin Shunda akiwa katika majukumu yake ya ufundishaji na uwezeshaji wa uongozi kwa walimu wakuu wa shule za msingi na sekondari wa Jiji la Dar es Salaam.
 Washiriki wa Semina hiyo wakifuatilia mafunzo hayo kwa umakini mkubwa.
 Afisa Mkuu wa Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika kutoka Manispaa ya Kinondoni,Saleh Hijja Mohamed (kushoto) akigawa cheti kwa mmoja wa washiriki wa semina ya siku tatu ya mafunzo ya uongozi kwa walimu wa shule za msingi na sekondari wa Jiji la Dar es Salaam leo. Semina hiyo imefanyika katika Kituo cha Walimu cha Mzimuni kilichopo Magomeni Mapipa. Kulia wanaoshuhudia ni Afisa Mkuu wa Miradi wa Shirika lisilo la Kiserikali la British Council,Atiya Sumar na Meneja Miradi wa Shirika hilo,Ephraim Kapungu. Picha na Elisa Shunda
 Afisa Elimu Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni,Kiduma Mageni akimpongeza mmoja wa washiriki wa semina ya siku tatu ya mafunzo ya uongozi kwa walimu wa shule za msingi na sekondari wa Jiji la Dar es Salaam leo.
Mgeni rasmi, Afisa Mkuu wa Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika kutoka Manispaa ya Kinondoni,Saleh Hijja Mohamed (katikati) akiwa na viongozi wa shirika la British pamoja na walimu wakuu wa shule za msingi na sekondari katika picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa semina ya siku tatu ya mafunzo ya uongozi kwa walimu hao wa Jiji la Dar es Salaam.

No comments: