Advertisements

Wednesday, April 17, 2019

Shirika la Wafanyakazi wa Kujitolea wa Kimarekani la Peace Corps lawaapisha Wafanyakazi wa Kujitolea 59 wa sekta za Afya na Kilimo

Kaimu Balozi wa Marekani nchini Dk. Inmi Patterson akiwaapisha wafanyakazi wapya wa kujitolea wa Peace Corps 59 ili kuanza utumishi wao wa miaka miwili nchini Tanzania katika hafla iliyofanyika tarehe 17 Aprili 2019 katika ukumbi wa CCT Kilakala Morogoro. Wafanyakazi hawa wa kujitolea wa Kimarekani watakao pangiwa kuhudumu katika wilaya 35 nchini, watafanyakazi na jamii katika sekta za afya na kilimo. Hafla ya kuapishwa kwao ilihudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. Mwita Waitara, Mkurugenzi Mkazi wa Peace Corps Tanzania Dk. Nelson Cronyn, wafanyakazi wa kujitolea wa Peace Corps waliohudumu hapo zamani pamoja na maafisa kutoka mashirika mengine yanayojihusisha na wafanyakazi wa kujitolea.

Ubalozi wa Marekani
Dar es Salaam
TANZANIA
17 April, 2019
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Shirika la Wafanyakazi wa Kujitolea wa Kimarekani la Peace Corps lawaapisha Wafanyakazi wa Kujitolea 59 wa sekta za Afya na Kilimo

Dar es Salaam, TANZANIA. Tarehe 17 Aprili 2019, Kaimu Balozi wa Marekani nchini Dk. Inmi Patterson aliongoza hafla ya kuapishwa kwa wafanyakazi wa kujitolea wa Kimarekani wa Peace Corps wapatao 59 watakaohudumu nchini Tanzania kwa miaka miwili katika sekta za Afya na Kilimo. Wafanyakazi hawa watapangiwa kufanyakazi katika wilaya 35 nchini kote Tanzania.

Kaimu Balozi Patterson aliongoza kiapo rasmi cha wafanyakazi hao wapya wa kujitolea mbele ya mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. Mwita Mwikwabe Waitara. Hafla hiyo ilihudhuriwa pia na viongozi wa serikali, wafanyakazi wa kujitolea wa zamani wa Peace Corps, wawakilishi wa taasisi wabia na wanafamilia wa familia za Kitanzania ambazo wafanyakazi hawa wa kujitolewa waliishi nazo.

Kaimu Balozi Patterson aliwaeleza wafanyakazi wapya wa kujitolea kuwa: “Kupitia programu hii mtaweza kuleta mabadiliko kwa Watanzania mtakaofanya nao kazi n ahata kwenu ninyi wenyewe.Wakati ambapo ninyi mnaweza kuwa Wamarekani wa kwanza kukutana na kufanya kazi na wafanyakazi wenzenu na majirani zenu wa Kitanzania, ni dhahiri kwamba katika mawazo yao mtaendelea kuwa wawakilishi wa watu wa Marekani na ubia wa muda mrefu kati ya Wamarekani na Watanzania.”

Peace Corps ni taasisi ya Serikali ya Marekani iliyoanzishwa na Rais John F. Kennedy mwaka 1961 ambayo hivi sasa inahudumia zaidi ya wafanyakazi wa kujitolea zaidi ya 7,000 katika zaidi ya nchi 70 duniani. Kwa zaidi ya miaka 50, Peace Corps imekuwa taasisi inayoendesha shughuli za mabadilishano ya kiufundi na kitamaduni zisizoegemea mrengo wowote wa kisiasa na kidini. Peace Corps ina dhamira ya kukuza amani na urafiki duniani kwa kutekeleza malengo matatu yafuatayo:

Kutoa wafanyakazi wa kujitolea wa Kimarekani watakaochangia kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika nchi itakayohitaji wafanyakazi hao:

Kukuza uelewa kuhusu Wamarekani miongoni mwa watu katika jamii zinazohudumiwa na Wafanyakazi wa kujitolea;

Kuimarisha uelewa wa Wamarekani kuhusu dunia na watu wake.

Zaidi ya wafanyakazi wa kujitolewa wa Peace Corps 3000 wamehudumu nchini Tanzania toka mwaka 1961. Peace Corps hutoa wafanyakazi wa kujitolea wa Kimarekani wenye utaalamu katika nyanja mbalimbali ambao hupangiwa kufanyakazi katika jamii wakifundisha katika shule za sekondari (hisabati, sayansi na Kiingereza), wakitoa elimu ya afya na utunzaji wa mazingira.

Kwa taarifa zaidi, tafadhali piga simu Ofisi ya Habari ya Ubalozi wa Marekani Dar es Salaam kupitia: +255 22 229-4000 au barua pepe: DPO@state.gov.

No comments: