Advertisements

Wednesday, April 17, 2019

Dkt. Ndumbaro afanya mazungumzo na Mwakilishi wa JICA nchini

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Dkt. Damas Daniel Ndumbaro (Mb.), amefanya mazungumzo na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) nchini, Bw.Naofumi Yamamura, hivi karibuni katika ofisi za wizara Dodoma. Mazungumzo hayo, yanalenga kuimarisha ushirikiano wa Tanzania na Japan kupitia shirika hilo katika masuala ya miundombinu. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Daniel Ndumbaro, akisalimiana na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) nchini, Bw. Naofumi Yamamura,mara baada ya kuwasili katika ofisi za wizara. 
Mazungumzo yakiendelea. 
Afisa Mambo ya Nje wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashiriki, Bi. Bertha Makilagi na Katibu wa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Charles Faini, wakifuatilia mazungumzo hayo. 
Afisa Mwandamizi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA), Takusaburo Kimura, akifafanua jambo wakati wa mazungumzo hayo. 
Wawakilishi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) nchini, Bw. Naofumi Yamamura na Afisa Mwandamizi wa shirika hilo, Bw. Takusaburo Kimura, wakimsikiliza Naibu Waziri wa mambo ya Nje na Ushirkiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Daniel Ndumbaro (hayupo pichani).

No comments: