Mkurugenzi wa Mawasiliano kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Emmanuel Buhohela.
“Sisi kama Wizara mawasiliano yote huwa yanafanyika kwa Waraka maalumu wa Kidplomasia, ndio maana kuna Ubalozi kwahiyo kama kungekuwa na jambo lolote wangetueleza kwa kutumia njia hiyo, na hadi sasa hatujapata ujumbe wowote na hatuwezi kuzungumzia vitu ambavyo vinasemwa kwenye mitandao,” alisema Buhohela.
Hayo ni baada ya taarifa zilizosambaa zinazodai kwamba Serikali ya Rais Donald Trump wa Marekani kuwa na mpango wa kuziongeza nchi nyingine saba, ikiwemo Tanzania kwenye orodha ya nchi ambazo, Raia wake wamewekewa vikwazo vya kuingia nchini humo.
No comments:
Post a Comment