Advertisements

Wednesday, March 25, 2020

Niyonzima Afunguka Maisha Yake Ndani ya Yanga

Kiungo mchezeshaji fundi wa Yanga, Mnyarwanda Haruna Niyonzima, akisani kitabu cha wageni leo Machi 25, 2020, katika ofisi za Global Group zilizopo Sinza-Mori jijini Dar es Salaam. GPL
KIUNGO mchezeshaji fundi wa Yanga, Mnyarwanda Haruna Niyonzima leo Machi 25, 2020, amefika katika ofisi ya Global Group zilizopo Sinza-Mori jijini Dar es Salaam ambapo katika mahojiano kupitia Global TV Online amefunguka kuwa anafurahia maisha mazuri tangu ametua nchini Tanzania, mwaka 2012 akitokea APR ya Rwanda.
Mwandishi wa Gazeti la Championi, Wilbert Molandi, akimuonyesha Haruna Niyonzima sehemu ya kunawa sanitizer.
…Wakiongea jambo wakati akiendelea kutembezwa ndani ya ofisi.
Mhariri wa Gazeti la Ijumaa na Ijumaa Wikienda, Sifael Paul (kushoto) akijiandaa kumkabidhi Gazeti la Ijumaa Niyonzima.
Mhariri Mtendaji wa Global Publishers, Saleh Ally (kushoto) akiongea na Ninyonzima ofisini kwake.
…Wakiongea jambo.
Mwandishi wa Global Publishers, Said Ally (kulia), akimkabidhi Niyonzima gazeti la Betika.
Mhariri msadizi wa gazeti la Spoti Xtra, Martha Mboma, akimkabishi gazeti Niyonzima.

No comments: