Thursday, April 9, 2020

DC WA SINGIDA AJA NA OPERESHENI TOKOMEZA CORONA

Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskasi Muragili akiwa ndani ya basi la Kampuni ya Kiazi Kitamu akiwaeleza abiria mbinu za kujikinga na Virusi vya Corona (COVID-19) alipokuwa kwenye Operesheni maalum ya Tokomeza Corona Katika Manispaa ya Singida kwenye Kituo Kikuu cha mabasi. (Picha na. Peter Kashindye).
1 Madereva na Mawakala wa mabasi kwenye Kituo Kikuu cha mabasi ya Mkoa wa Singida (Misuna) wakionyesha jinsi ya kutumia vitakasa mikono ili kukabiliana na ugonjwa wa Corona (COVID-19) kwa Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskasi Muragili (Hayupo pichani) alipofanya Operesheni Maalum ya Tokomeza Corona Katika Manispaa ya Singida kuona utekelezaji wa maagizo ya Serikali ya kujikinga na ugonjwa huo (Picha na. Peter Kashindye).
Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskasi Muragili (aliyenyanyua mkono) akihoji uelewa wa kujikinga na virusi vya Corona (Covid-19) mahali pa kazi kwenye maduka ya kuuzia nyama alipofanya Operesheni Maalum ya Tokomeza Corona Katika Manispaa ya Singida kwenye Soko Kuu la Singida Mjini. (Picha na. Peter Kashindye).

No comments: