Advertisements

Tuesday, June 22, 2021

BALOZI MULAMULA AKUTANA NA MWAKILISHI MKAZI WA UNDP JIJINI DODOMA

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Mhe. Cristine Musisi (kushoto) ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza huku Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Mhe. Cristine Musisi akimsikiliza ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Mhe. Cristine Musisi baada ya kumaliza mazungumzo yao ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (katikati) akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Mhe. Cristine Musisi (kushoto) huku Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Mteule Makocha Tembele akishuhudia mazungumzo hayo yaliyofanyika katika mji wa Serikali jijini Dodoma.

**************************

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (MB) amekutana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Mhe. Cristine Musisi ofisini kwake Mtumba jijini Dodoma.

Katika mazungumzo hayo Viongozi hao wamejadiliana na kukubaliana kuendelea kuimarisha mahusiano kati ya UNDP , Wizara ya Mambo ya Nje na Serikali ya Tanzania ili kuhakikisha lengo la kupatikana kwa maendeleo linafikiwa kwa pamoja.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mulamula alimuhakikishia Bibi Musisi utayari wa Tanzania katika kuimarisha mahusiano na UNDP na kumueleza kuwa Serikali ya Tanzania imejipanga kutekeleza Diplomasia ya Uchumi kwa vitendo.

Mhe. Waziri pia amemuhakikishia Bibi Musisi kuwa Wizara yake inatilia mkazo kauli ya Serikali ya kuvutia na kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji na kufanya biashara nchini ili kuvutia wawekezaji na wafanya biashara kuja kuwekeza nchini kwa maendeleo ya Taifa.

Mhe Waziri alisisitiza kuwa Wizara inatilia mkazo pia suala la kuwajengea ujuzi wataalamu wake katika maeneo ya teknolojia ya habari na mawasiliano ili kwenda na wakati na hivyo kuendesha na kushiriki mikutano kwa njia ya mtandao hasa wakati huu wa ugonjwa wa CCOVID 19, ujuzi wa kufanya uchambuzi na namna bora ya kuwasiliana ili kuhakikisha Tanzania inanufaika na utekelezaji wa diplomasia ya uchumi..

Naye Mwakilishi Mkazi wa UNDP Mhe. Musisi alimuhakikishia Mhe. Waziri Mulamula kuwa UNDP ipo tayari na itaendelea kushirikiana na Wizara kwa karibu na Wizara ikiwa ni pamoja na kutoa wataalam na mafunzo kwa watendaji wa Serikali ili kuendeleza ujuzi wa watendaji serikalini na kuwafanya kutoa huduma bora zaidi kwa Taifa na wananchi wake.

Amesema UNDP itandelea kusaidia utoaji wa mafunzo, kuendesha na kusaidia miradi mbalimbali ya maendeleo kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania na Tanzania ujumla.

No comments: