Advertisements

Thursday, April 18, 2024

HALMASHAURI YA MPIMBWE YAGUSHI MHUTASARI WA VIKAO WA UPITISHAJI BAJETI



*Kikao cha kugushi walipeleka hazina ajili ya hiyo bajeti
Fedha zilizobadilishwa matumizi bila kuidhinishwa na mamlaka husika na utumiaji wa nyaraka za kubadili matumizi ya udanganyifu kiasi cha Sh. bilioni 4.88

Ukaguzi ulibaini kwamba mamlaka nne za serikali za mitaa zilibadilisha matumizi ya kiasi cha Sh.bilioni 4.88bila kupata idhini kutoka kwa mamlaka husika, zikiwamo Baraza la Madiwani na Waziri wa Fedha.

Halmashauri iliyobanika katika ripoti ya CAG kati ya hizo ni Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe mkoani Katavi ilipanga kutumia bajeti ya kiasi cha Sh.bilioni 7.06 kwa
ajili ya kulipa mishahara hata hivyo, bajeti hiyo ilibadilishwa kwa
kuongeza kiasi cha Sh.bilioni 2.07. Kati ya kiasi kiasi hicho kilichotengwa Sh.bilioni 1.61 tu ndizo zilizotumika.

Pia ukaguzi ulibaini nyaraka za mihutasari ya kikao cha kamati ya fedha, mipango na uongozi kilichofanyika tarehe 5 Juni 2023 zilighushiwa na kuwasilishwa Hazina kwa ajili yakuombakibali cha kubadili vifungu vya bajeti ya mishahara, ingawa kikaohicho hakikufanyika kama inavyoelezwa kwenye.

Hii ni kinyume na Kifungu Na.41(2) cha Sheria ya Bajeti, [Sura ya 439], ambacho kinaeleza kwamba ofisa masuuli hatabadilisha matumizi ya fedha endapo fedha hizo zinapaswa kuhamishwa kwenda kwa mtu au kwa taasisi zingineza serikali.

Maombi ya kubadilisha matumizi ya fedha yanapaswa kuambatishwa na taarifa inayoelezea kikamilifu sababu za ukosefu wa fedha zilizoidhinishwa awali. Baada ya kujadiliwa na kamati ya fedha mipango na uongozi, maombi hayo huwasilishwa kwa Baraza la Madiwani kwa ajili ya kuidhinishwa.

Pia, Kifungu cha 41(1&2) cha Sheria ya Bajeti, [Sura ya 439], kinaruhusu ofisa masuuli, kwa idhini ya waziri, kubadili matumizi kutoka kwenye matumizi yaliyoidhinishwa.

Hata hivyo, Ofisa masuuli hatabadili matumizi ya fedha katika mazingira yafuatayo ambapo fedha zimetengwa kwa ajili ajili ya kazi maalum fedha zilizotengwa kwa ajili ya kuhamishwa kwenda kwa mtu au taasisi zingineza serikali fedha zilizotengwa kwa ajili ya matumizi ya shughuli zinazohusiana na maendeleo fedha zilizotengwa kwa ajili ya mishahara kwenda kwenye matumizi mengine yasiyo ya mishahara na uhamishaji wa fedha mwingineo unaweza kusababisha ukiukwaji wa kanuni za kifedha.

No comments: