ANGALIA LIVE NEWS

Saturday, March 22, 2025

CHIFU WA MBEYA ROCKETI MASOKO MWANSHINGA AKEMEA WANAPANGA KUZUIA WANANCH...

CHIFU WA MBEYA ROCKETI MASOKO MWANSHINGA AKEMEA WANAPANGA KUZUIA

 WANANCHI KUJITOKEZA KWENYE UCHAGUZI




Chifu wa Mkoa wa Mbeya, Rocketi Masoko Mwanshinga, amewataka wananchi wote wa mkoa huo

 kutumia haki yao ya kikatiba kujiandikisha na kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi Mkuu wa 2025.



Chifu Mwanshinga amekemea vikali wale wote wanaotaka kuwazuia wananchi kushiriki katika mchakato

 wa uchaguzi, akisema Mungu atawapa usingizi na hawataweza kuzuia uchaguzi kufanyika.



Amesisitiza kuwa kila raia ana haki ya kupiga kura na kupigiwa kura bila hofu wala vizuizi vyovyote. A

idha, Chifu Mwanshinga amemuombea Rais Samia Suluhu  Hassan apate ushindi wa kishindo, akisema kuwa uongozi wake umekuwa wa neema kwa Watanzania.




Amewataka wakazi wa Mbeya kuungana kwa mshikamano na kuhakikisha wanatekeleza wajibu wao wa kidemokrasia ili kuchagua viongozi watakaosukuma mbele maendeleo ya Tanzania.


No comments: