Na Issa Mwadangala
Askari Polisi wa kike Mkoani Songwe wajidhatiti kuendelea kiuchumi na kuwa na afya bora ya akili na mwili kwa kufanya semina, sherehe na midahalo mbalimbali ili kuendelea kujiimarisha kiuchumi.
Kauli hiyo imetolewa Aprili 22, 2025 na Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi Wanawake Mkoa wa Songwe (TPF- Net) Mkoa wa Songwe Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) Akama Shaaban katika kikao cha mipango mikakati kuelekea kuwaaga wastaafu, kuyafariji makundi yenye uhitaji, kujengewa uelewa kuhusu elimu ya afya ya akili, uzazi na magonjwa yasiyoambukiza pamoja na kufanya sherehe ya TPF Net Gala inayofanyika kila mwaka.
ACP Akama alisema, wakati wakielekea kwenye sherehe hiyo inayotarajiwa kufanyika hivi karibuni, wamejipanga kupata elimu pamoja na kuwafariji wahitaji katika jamii.
No comments:
Post a Comment