Mchezaji matata wa Ivory Coast Didier Droga ameshinda tuzo la mwanasoka bora zaidi barani Afrika mwaka 2009.
Drogba aliingiza mabao matano wakati Ivory Coast ilipofuzu kwa kombe la dunia na vile vile kuingizia kilabu yake ya bao katika fainali ya kombe la FA.
Mwenzake wa kilabu hiyo Michael Essien na mchezaji wa Cameroon Samuel Eto'o waliteuliwa kuwania tuzo hiyo.
Drogba, aliyefikisha umri wa miaka 32, hapo jana, amewahi kushinda tuzo hilo mwaka wa 2006.
Timu ya taifa ya Algeria ilitajwa kuwa timu bora zaidi mwaka huu katika sherehe iliyofanyika mjini Accra, Ghana.
No comments:
Post a Comment