
Wakati mwingine unaweza kusema maisha haya si ya kuwalaumu wanasiasa wetu tu, pengine tumuombe na Mungu atufungulie neema zake, kwani hali ya maisha ni ngumu sana kwa wanachi wengi wa vijijini na ile dhana ya maihsa bora kwa 'kila mtanzania' ni msemo ambao unapoteza maana kila kukicha. Munagalie huyo bibi pichani juu, yumo ndani ya kijumba chake, ni asubuhi ameamka na kutafakari akiwa juu ya kijitanda chake, 'leo nitaishije,!

...ndiyo kumeshakucha na ni lazima aamke kutafuta riziki...anaanzia wapi!

.....mchana umefika, watoto lazima wale na huu ndiyo mlo wao wa siku...ukiingalia familia hii kwa makini huhitaji kuambiwa ina matatizo kiasi gani.
PICHA: Hisani ya mdau Emmanuel Abel
Chanzo:GPL
1 comment:
Safari bado ni ndefu sana kwa nchi yetu. Nimesoma gazeti la majira leo nimona wamesema wanafunzi wa shule ya misewe Ilala jijini Dar wanalazimika kubeba kanga na viloba ili wakakalie shuleni, sasa hapo dar tu ni hivyo na vijijini itakuwaje,tumezungukwa na miti lakini mh! anajua mungu. Familia nyingi wanaishi kwa neema ya mungu tu,sasa kama huyo bibi wa watu ndo kakata tamaa kabiza.
Post a Comment