ANGALIA LIVE NEWS

Monday, May 16, 2011

Mkuu wa IMF atakana mashitaka

International Monetary Fund Managing Director Dominique Strauss-Kahn attends the IMF/World Bank spring meetings in Washington (File Photo - April 16, 2011)
Anatazamiwa kufikishwa mahakamani kufunguliwa mashitaka rasmi
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa IMF, Dominique Strauss-Kahn, anatazamiwa kufikishwa mahakamani kufunguliwa mashitaka rasmi mjini New York baada ya polisi kumtia nguvuni kwa madai ya kujaribu kumbaka mwanamke mmoja katika hoteli mjini New York.
Wakili wa Bwana Strauss-Kahn anasema mkuu huyo wa IMF atakana mashitaka.
Alikamatwa Jumamosi usiku akiwa ndani ya ndege ya shirika la Air France kwa safari ya kwenda Ufaransa. Polisi wanasema saa chache kabla ya hapo Strauss-Kahn alijaribu kumbaka mwanamke mmoja msafisha chumba katika hoteli ya Sofitel mjini New York.

Mwanamke huyo ambaye angali anahojiwa na polisi anadai kuwa aliingia chumbani kwa Strauss-Kahn kufanya usafi akidhani hakuna mtu ndani. Lakini ghafla, anasema, Strauss-Kahn alitokea chumba kingine akiwa uchi na kujaribu kumvuta afanye naye mapenzi. Mwanamke huyo aliweza kuponyoka na kukimbia kuripoti kwa maafisa wa hoteli.
Haifahamiki kama Bwana Strauss-Kahn kama afisa wa juu wa shirika la kimataifa ana kinga ya kidiplomasia lakini polisi wanasema hajasema lolote kuhusu kudai kinga hiyo
CHANZO:VOA

No comments: