PETE ambayo ni Diamond ya Ukweli
Wachumba wakiwa na baadhi ya marafiki zao na familia
Mr Chabaka akitoa pete.
URBAN PULSE CREATIVE inawaletea picha ya sherehe fupi ya Uchumba iliyofanyika Jumamosi Tarehe 22 Oktoba 2011 kati ya Naibu Balozi wetu Mh.Chabaka na Bi Irene. Sherehe hii ilihudhuriwa na baadhi ya ndugu pamoja na marafiki wa karibu waliojumuika kwa pamoja kushuhudia tukio hili muhimu katika safari yao ya kuelekea kwenye ndoa.
Vazi alilovaa Bi Irene limebuniwa na kutengenezwa ramsi na Anna Lukindo. Tarehe na pamoja taratibu zote za harusi zitatolewa rasmi muda muafaka utakapowadia.
Hivyo basi Urban Pulse Creative na Miss Jestina George tunapenda kuwapa hongera na fanaka katika penzi lao na maisha yao ya baadae, Mungu Awabariki.
Asanteni,

1 comment:
CONGRATULATIONS MY DEARS..NASUBIRIA PICHA ZA HARUSI KWA HAM" GOD BLESS YOU BOTH :)
Post a Comment