Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hadji Mponda na Naibu wake, Dk Lucy Nkya.
Midraji Ibrahim, Dodoma
KAMATI ya wabunge wa CCM imemtaka Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hadji Mponda, Naibu wake, Dk Lucy Nkya na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Blandina Nyoni, kujiuzulu kwa kile walichoeleza kuwa wao ni chanzo cha mgomo wa madaktari unaendelea nchini.Wakati hayo yakijitokeza, Bunge limejitosa kusuluhisha mgogoro huo kwa kusikiliza pande zote zinazohusika; Serikali na madaktari.
KAMATI ya wabunge wa CCM imemtaka Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hadji Mponda, Naibu wake, Dk Lucy Nkya na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Blandina Nyoni, kujiuzulu kwa kile walichoeleza kuwa wao ni chanzo cha mgomo wa madaktari unaendelea nchini.Wakati hayo yakijitokeza, Bunge limejitosa kusuluhisha mgogoro huo kwa kusikiliza pande zote zinazohusika; Serikali na madaktari.
Pia, wabunge hao wa CCM wanadaiwa kuishutumu Serikali kwa kuchukua muda mrefu kabla ya kuingilia kati masuala muhimu ya taifa likiwamo hili la mgomo.Taarifa za uhakika kutoka ndani ya kikao hicho kilichofanyika juzi usiku, zimeeleza kuwa wabunge hao walidai kuwa viongozi hao wamekuwa kiini cha mgogoro wa madaktari kwa kushindwa kutoa suluhisho na kusababisha vifo vya raia wasio na hatia.
Mbunge wa Sikonge, Said Nkumba (CCM), anadaiwa kuwa wa kwanza kutaka viongozi hao wajiuzulu na wakikaidi wawajibishwe na mamlaka husika yani Rais.
Pendekezo hilo liliungwa mkono na Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka aliyehoji hatua ya Serikali kuchelewa kutoa uamuzi kuhusu masuala ya kitaifa.Sendeka anadaiwa alituhumu Serikali kushindwa kuingilia kati haraka migogoro inayojitokeza nchini na kusubiri hadi maafa yatokee.
Kauli ya Serikali bungeni
Akiwasilisha kauli ya Serikali bungeni jana, Dk Mponda huku akitoa mlolongo wa historia ya mgomo huo, alisema Januari 30, mwaka huu, Serikali iliunda kamati ya kushughulikia maazimio yaliyowasilishwa na madaktari kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Dk Mponda alisema kamati hiyo itayachambua na kutoa maoni na mapendekezo yatakayosaidia Serikali kumaliza mgogoro huo wa watumishi wa sekta ya afya na kwamba, tayari imeanza kazi.
“Kamati hiyo inajumuisha wajumbe kutoka Ofisi ya Rais (Utumishi), Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Wizara ya Fedha, Tughe, mwakilishi wa madaktari, mwakilishi wa wauguzi, Tamisemi, Mwanasheria Mkuu na Wizara ya Kazi na Maendeleo ya Ajira,” alisema.Waziri Mponda alisema kamati hiyo imepewa hadidu za rejea zinazoainisha masuala yanayotakiwa kufanyiwa kazi na itafanya kazi kwa wiki mbili.
Hadidu za rejea zilizotolewa ni kupitia hali ya sasa ya maslahi ya madaktari na watumishi wengine wa kada za afya; kupitia, kufanya uchambuzi wa kina wa madai ya madaktari na watumishi wengine wa kada hiyo; kubaini gharama za utekelezaji wa madai ya maslahi ya madaktari na watumishi wengine wa sekta hiyo.
Nyingine ni kupendekeza na kushauri namna bora ya kushughulikia madai ya watumishi hao kipindi cha muda mfupi, muda wa kati na muda mrefu na kuandaa taarifa na kuiwasilisha kwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii.
Awali, Dk Mponda alisisitiza kuwa mgomo huo siyo halali kwa sababu kisheria madaktari hawaruhusiwi kugoma.
“Masharti haya yanaainishwa katika kifungu cha 77 (1)(a) cha Sheria ya Ajira na Uhusiano kazini (Na.6 ya mwaka 2004) ambayo inazuia kugoma watumishi wote walio katika ‘huduma muhimu’ (Necessary Services),” alisema.
Dk Mponda alisema madaktari wapya wanaoajiriwa wanalipwa 957,700, huku watumishi wa kada nyingine kama wahandisi wanaanza na Sh600,000 na wahasibu wanaanza na mshahara wa Sh469,200.
Alisema utekelezaji wa pendekezo la madaktari la kulipwa mshahara wa Sh3.5 milioni kwa mwezi kwa daktari atakayeanza kazi, utalazimu Serikali kurekebisha viwango vya mishahara kwa watumishi wote wa afya na kada zingine na mhudumu wa sekta hiyo atakuwa analipwa Sh670,316 na mshahara wa juu wa kada hiyo utakuwa Sh8,145,573.
“Utekelezaji wa pendekezo hili utaigharimu Serikali Sh83,508,834,430 kwa mwezi ambayo ni sawa na Sh417,544,172,150 kwa kipindi kilichobaki cha miezi mitano mwaka huu wa fedha,” alisema.
Hata hivyo, Dk Mponda alisema hivi sasa hali ni nzuri isipokuwa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (Moi), ambako alidai wanawasiliana na Wizara ya Ulinzi na JKT kwa ajili ya kupeleka madaktari wanajeshi.
Kauli za wabunge
Mbunge wa Kasulu Mjini, Moses Machali (NCCR-Mageuzi), alisimama na kutumia kanuni ya 53 (a) ambayo inatoa ruhusu ya kutengua kanuni yoyote, huku akitaka kutengeuliwa kwa kanuni 49 (2) inayozuia kauli inayopelekwa na Serikali kujadiliwa bungeni.
Hoja hiyo iliungwa mkono na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema), aliyesema kauli hiyo ni muhimu sana, inayohusu afya za Watanzania na sekta ambayo inatengewa fedha nyingi lazima ijadiliwe.
Awali, Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (Chadema), akitumia kanuni ya 5 (1) na Ibara ya 63 (2), alitaka kanuni ya 49 (2) kutenguliwa kutokana na unyeti wa kauli hiyo.
“Serikali ni mmoja wa watuhumiwa kutokana na waziri, naibu wake na katibu mkuu kwa utendaji wao mbovu …itapelekea tushindwe kuijadili na tusiwawajibishe kwa ubovu wao,” alisema Mnyika.
Kauli ya Naibu Spika
Akitoa mwongozo wake, Naibu Spika, Job Ndugai, alisema hoja hizo hazikuungwa mkono na wabunge kwa hiyo wanabanwa na kanuni zao, huku akiwataka watakapokuwa wazinafanya marekebisho kuangalia kanuni hiyo.
Hata hivyo, Ndugai alisema suala la mgomo wa madaktari ni zito na kwamba, tatizo lililojitokeza ni kusikiliza upande mmoja wa Serikali kwa sababu, madaktari hawawezi kwenda kusimama bungeni kueleza madai yao.
“Waziri ametueleza kuwa wameunda kamati ya kupitia madai ya madaktari, nakumbuka mojawapo ya madai yao ambayo Serikali haikutaja hapa na hiyo nina uhakika hiyo kamati haitasema ni kwamba, Wizara ya afya kuna baadhi ya watendaji wenye uwezo wa kiutendaji wana kauli mbaya na dharau,” alisema Ndugai na kuongeza:
“Hiyo haimo. Uamuzi wa kuhusu jambo hili nalipeleka Kamati ya Huduma za Jamii, ilifanyie kazi haraka kwa kuita pande zote zinazohusika ziweze kueleza madai yao na tutapata mwafaka haraka.”
Hata hivyo, Dk Mponda alisema hivi sasa hali ni nzuri isipokuwa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (Moi), ambako alidai wanawasiliana na Wizara ya Ulinzi na JKT kwa ajili ya kupeleka madaktari wanajeshi.
Kauli za wabunge
Mbunge wa Kasulu Mjini, Moses Machali (NCCR-Mageuzi), alisimama na kutumia kanuni ya 53 (a) ambayo inatoa ruhusu ya kutengua kanuni yoyote, huku akitaka kutengeuliwa kwa kanuni 49 (2) inayozuia kauli inayopelekwa na Serikali kujadiliwa bungeni.
Hoja hiyo iliungwa mkono na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (Chadema), aliyesema kauli hiyo ni muhimu sana, inayohusu afya za Watanzania na sekta ambayo inatengewa fedha nyingi lazima ijadiliwe.
Awali, Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (Chadema), akitumia kanuni ya 5 (1) na Ibara ya 63 (2), alitaka kanuni ya 49 (2) kutenguliwa kutokana na unyeti wa kauli hiyo.
“Serikali ni mmoja wa watuhumiwa kutokana na waziri, naibu wake na katibu mkuu kwa utendaji wao mbovu …itapelekea tushindwe kuijadili na tusiwawajibishe kwa ubovu wao,” alisema Mnyika.
Kauli ya Naibu Spika
Akitoa mwongozo wake, Naibu Spika, Job Ndugai, alisema hoja hizo hazikuungwa mkono na wabunge kwa hiyo wanabanwa na kanuni zao, huku akiwataka watakapokuwa wazinafanya marekebisho kuangalia kanuni hiyo.
Hata hivyo, Ndugai alisema suala la mgomo wa madaktari ni zito na kwamba, tatizo lililojitokeza ni kusikiliza upande mmoja wa Serikali kwa sababu, madaktari hawawezi kwenda kusimama bungeni kueleza madai yao.
“Waziri ametueleza kuwa wameunda kamati ya kupitia madai ya madaktari, nakumbuka mojawapo ya madai yao ambayo Serikali haikutaja hapa na hiyo nina uhakika hiyo kamati haitasema ni kwamba, Wizara ya afya kuna baadhi ya watendaji wenye uwezo wa kiutendaji wana kauli mbaya na dharau,” alisema Ndugai na kuongeza:
“Hiyo haimo. Uamuzi wa kuhusu jambo hili nalipeleka Kamati ya Huduma za Jamii, ilifanyie kazi haraka kwa kuita pande zote zinazohusika ziweze kueleza madai yao na tutapata mwafaka haraka.”
Mwananchi
No comments:
Post a Comment