Advertisements

Friday, December 14, 2012

KOFFI OLOMIDE AONGEA NA MEDIA



Bango alilotia wino Koffi Olomide.

Koffi Olomide akitoa vionjo vya moja ya wimbo wake mbele ya wanahabari,kulia kwake ni Mkurugenzi wa Mahusiano Serengeti Breweries,Nandi Mwiyombela akinogesha

Mkurugenzi wa Masoko kampuni ya SBL,Ephraim Mafuru akiuzumguza mbele ya Wanahabari mapema leo ndani ya hotel ya Serena Inn,kuhusiana na onesho la Mwanamuziki kutoka DRC-Congo,Koffi Olomide linalotarajiwa kufanyika kesho jumamosi kwenye viwanja vya Lidaz Club,Kinondoni jijini Dar.

Baadhi ya wafanyakazi wa SBL wakifurahia jambo

Mkurugenzi wa Mahusiano Serengeti Breweries,Nandi Mwiyombela akiwakaribisha wageni mbalimbali wakiwemo wanahabari kwenye mkutano uliohusu onesho la Mwanamuziki Koffi Olomide,ambalo limedhaminiwa na kampuni ya SBL kupitia kinywaji chake cha Tusker.

Mwanamuziki kutoka nchini DRC-Congo,Koffi Olomide akifafanua jambo mapema leo alipokuwa akizungumza na wanahabari (hawapo pichani),ndani ya hotel ya Serena kuhusiana na onesho lake atakalolifanya hapo kesho ndani ya viwanja vya Lidaz Club,Koffi amewaomba washabiki na wapenzi wake waje wajionee kazi kubwa atakayokuwa akiifanya jukwaani akiwa na vipaji vipya kabisa katika tasnia ya muziki wa dansi nchini Congo.
Kwa picha zaidi bofya read more

Mkurugenzi wa kampuni ya bia ya Serengeti,Bwa.Steve Gannon akimkaribisha Koffi Olomide (hayupo pichani) na pia aliwataka mashabiki na wapenzi wa mwanamuziki huyo wajitokeze kwa wingi na kushuhudia tukio hilo adhimu hapo kesho.

Mkurugenzi wa Clouds Media Group,Joseph Kusaga akiwashukuru Wadhamini wa onesho la Koffi Olomide pamoja na Wanahabari kwa ushirikiano mkubwa walioutoa katika kuhakikisha jamii inapata taarifa mbalimbali kuhusiana na ujio wa mwanamuziki huyo pamoja na onesho lenyewe.

Mkurugenzi wa Masoko kampuni ya SBL,Ephraim Mafuru akisalimiana mkono na Mwanamuziki wa Kimataifa Koffi Olomide.

Mkurugenzi wa Clouds Media Group,Joseph Kusaga pichani shoto akiwa ameambata na mgeni wake Koffi Olomide sambamba na Mkurugenzi wa SBL,Steve Gannon wakiwasili ndani ya ukumbi wa mikutano,Serena Hotel kwa ajili ya kuzungumza na Wanahabari kuhusiana na onesho litakalofanyika kesho kwenye viwannja vya Lidaz Club,Kinondoni jijini Dar.
Picha na Michuzijr.Blogspot.com

No comments: