Saturday, February 9, 2013

MASHINDANO YA BODABODA CUP KINONDONI YAZIDI KUSHIKA KASI, TEGETA YAPIGWA 3-0 NA KAWE

Wachezaji wa timu za waendesha Bodaboda kutoka Tegeta na Kawe, wakichuana kuwania mpira wakati wa ufunguzi wa mashindano ya Kombe la Bodaboda 'Bodaboda Cup' inayoendeshwa na Jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani. Katika mchezo huo timu ya Kawe imeibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Tegeta, mchezo uliofanyika katika uwanja wa Tanganyika Pakers Kawe jijini Dar es salaam leo.


Mashindano hayo yanashirikisha timu za mkoa wa kipolisi wa Kinondoni ambazo zinatoka katika maeneo ya Kimara, Kawe, Tegeta, Mabibo na Ubungo, ambapo wachezaji washiriki wa mashindano hayo wanatakiwa kuwa ni waendesha pikipiki za kupakia abiria tu 'Booda'. Awamu ya kwanza ya ligi hiyo ilikuwa na timu 32 na sasa ni awamu ya pili ambapo timu 16 zinashindana ili kupata timu 8 zitakazoshiriki Ligi ya Nane Bora na hatimaye kupata mshindi wa mashindano hayo ya 'Kinondoni Bodaboda Cup'.


Lengo la Mashindano hayo ni kuwakutanisha waendesha Bodaboda wote wa mkoa wa kipolisi wa Kinondoni ili waweze kufahamiana wao kwa wao, lakini pia ili jeshi la polisi Kikosi cha Usalama Barabarani liweze kuwaelimisha juu ya sheria za usalama Barabarani na Ulinzi Shirikishi kwa jamii.
Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Agatha Isack, akikagua timu kabla ya kuanza kwa michezo hiyo leo kwenye uwanja wa Tanganyika Pakers jijini Dar es salaam.
Mkaguzi msaidizi wa Jeshi la polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Agatha Isack akikagua timu.
Mkaguzi msaidizi wa Jeshi la polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Agatha Isack, akimtakia uchezeshaji mwema mshika kibendera wa kushoto Hamis Pondamali kabla ya kuanza kwa michezo hiyo leo kwenye uwanja wa Tanganyika Pakers jijini Dar es salaam.
Timu ya Kawe ikiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kwa mchezo huo na kupata mawaidha mawili matatu.
Kikosi cha timu ya Tegeta kikiwa katika picha ya pamoja kalba ya kuanza kwa mchezo huo timu hiyo imefungwa magoli 3-0 na timu ya Kawe.
Baadhi ya mashaifuatilia mchezo huo.
Wachezaji wa timu za Kawe na Tegeta wakiwania mpira uliojuu wakati wa mchezouliokutanisha timu hizo leo kwenye uwanja wa Tanganyika PakersKawe jijini Dar es salaam
Kutoka kulia ni Aghata Isack Mkaguzi Msaidizi Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Esther Ngaja Mkaguzi Msaidizi Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Refarii wa mchezo huo Geofrey Mwamboneke, Mshika Kibendera Hamis Pondamali, Mshika Kibendera Mwanahamisi Matiku, ASP. Emilian Kamuhanda Insp.Soud Ramadhan na Mratibu wa kombe hilo Ernest Mbaga wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo uliofanyika kwenye uwanja wa Tanganyika Pakers leo,
Mashabiki wakijikinga na jua huku wakifuatilia mchezo huo.

No comments: