Thursday, May 23, 2013

UGONJWA WA KISUKARI

Kisukari ni ugonjwa unaosababishwa na kuzidi kwa kiwango cha sukari mwilini, kunakoweza kusababishwa na ulaji mwingi wa sukari au kushindwa kwa kongosho (pancrease) kuzalisha kichocheo cha insulin ambacho ndiyo hufanya kazi ya kurekebisha kiwango cha sukari kwenye damu.
Ugonjwa huu ni miongoni mwa magonjwa yanayowatesa watu wengi duniani, huku ukielezwa kusababisha vifo vingi.
Aina za Kisukari
Ugonjwa huu wa kisukari, kitaalam umegawanyika katika makundi makuu matatu
1. Type 1 Diabetes Melitus (Juvenile)
Aina hii husababishwa na mwili hususan kongosho kushindwa kuzalisha insulin inayoratibu kiwango cha sukari mwilini.
2. Type 2 Diabetic Melitus (Adult)
Aina hii husababishwa na seli za mwili kushindwa kusanisi insulin ambayo tayari imeshazalishwa na kongosho na kuingizwa kwenye damu.
3. Gestational Diabetes
Aina hii ya ugonjwa huwapata akina mama wajawazito ambao hawakuwahi kuwa na tatizo hilo lakini kiwango cha damu kwenye miili yao kinaongezeka ghafla baada ya kushika ujauzito.
Aina nyingine za ugonjwa wa kisukari ni Congenital Diabetes ambayo hurithishwa, Steroid Diabetes, Monogenic Diabetes na nyingine nyingi.
Habari njema kwa wagonjwa wanaosumbuliwa na kisukari ni kwamba ugonjwa huo hivi sasa unatibika na wapo watu waliothibitishwa kupona kabisa. Hata hivyo, wagonjwa wasipowahishwa hospitali, hupatwa na matatizo mengine kama hypoglycemia, diabetic ketoacidosis na hyperosmolar coma. Pia husababisha matatizo ya moyo na mwisho husababisha kifo.

Global Publishers

No comments: