ANGALIA LIVE NEWS

Monday, June 24, 2013

AAR NA CRDB KUTOA MAFUNZO KWA WAFANYAKAZI WA NDANI


wishoni mwa wiki iliyopita AAR imetoa huduma ya bure ya mafunzo  kwa wafanyakazi wa nyumbani wa wawafanyakazi  wa CRDB .
Programu hii iliandaliwa na kutolewa na idara ya  huduma  ya washauri wa kampuni ya bima ya Afya ya  AAR (AAR Employees Wellness Program) kwa  nia ya kusaidia vijana hawa kuweza kujitambua,Kujithamini  na kufahamu jinsi ya kumudu majukumu yao kwa vizuri wanayopewa  na waajiri wao (wa CRDB),
“Tunawashukuru sana  AAR kwa kutoa huduma hii kwa wahudumu wetu wa nyumbani, kwakua  vijana hawa ndio wana muda  mwingi wa kukaa na nyumba pamoja na malezi ya watoto wetu kwa mda wote tunapokua kazini , natumai mafunzo haya yatakua na faida kwao na sisi pia kuwa na imani hata tuwapo makazini”. Alisema  Meneja Mafunzo CRDB  Agnes  Robert.
Mafunzo haya  yalihusika na mambo mengi  mbalimbali, baadhi ikiwa ni, kujitambua na kujithamini, heshima uwepo nyumbani, jinsi ya kulea watoto kiuanagalifu na kuwahudumia endapo wapatapo matatizo ya kiafya na mengineyo, vitu muhimu vya kuzingatia ndani ya nyumba ,Vitu visivyopaswa kufatwa.
“Kwakweli leo tumefurai sana kuja hapa CRDB nakupewa mafunzo na kampuni ya AAR , kwanza kabsa tumepanuka kimawazo, mambo mengi tulkua hatuyajui, na mengine hatukua tunadhani yanaumuhimu lakini leo tunashkuru AAR kwa kutusaidia kuyaelewa na pia kujithamini , kujikubali na kupenda kazi zetu alisema mmoja kati ya wafanyakazi wa nyumbani”.  Mariam Kayege
Programu hii inategemea kufanyika tena kwa mara nyingine kwenye makao makuu ya CRDB, na hapo baadae  pia kwa kampuni  na mashirika mengine mbali mbali nchini.

No comments: