Saturday, November 23, 2013

DIAMOND HANA HADHI YA KUTEMBEA NA MIMI-LULU AJITIRIRISHA



Msanii wa filamu bongo,na mwenye jina kubwa kuliko umri wake,Elizabeth Michael aka LULU, ameonesha msimamo mkali baada ya msanii wa bongo fleva mwenye jina la madini expensive Naseeb Mohamed au DIAMOND kufanya kila aina ya mbinu ikiwemo ile ya kutaka kumuagizia msanii huyo gari expensive aina ya nissan murrano yenye thamani ya shiling million zaidi ya 60,ambapo hata hivyo mbinu yake iyo imeonekana kugonga mwamba baaada ya Lulu kukataa kata kata kutoka na staa huyo anayetamba na ngoma ya my number one.
Kwa kumaanisha kuwa hataki kutoka na staa huyo, Lulu alilazimika kubadilisha namba ya simu yake ya mkononi ili kuepuka usumbufu kutoka kwa bwana mdogo huyo ambaye kila kukicha amekuwa akiwindwa na wasichana warembo ili tu waonje sukari yake. 

Pia inasemekana lengo la diamond kutaka kutoka na Lulu ni kutaka kukuza jina lake(kiki) kwa kuwa anaamini staa huyo ana jina kubwa na lenye mvuto hivyo kumfanya na yeye aogelee kwenye dimbwi la umaarufu na kuongelewa zaidi na watu,na kuwa ishu iyo ndo itakuwa habari ya mujini yaan yeye kutoka na lulu.

Baadhi ya watu wameonyesha kushangzwa sana na msimamo mkali wa binti huyo,kwa kuwa waliamini hakuna staa yeyote bongo mwenye ubavu wa kupindua kwa diamond,kama ilivyokuwa kwa Wema,Jokate,Aunt,Wolper na baadhi ya mastaa ambao dogo huyo aliwamega kiulaini. 

Watu wanahaha kumjua mwanaume anayempa jeuri Lulu hadi kufikia hatua ya kuchomoa kwa diamond..

12 comments:

Anonymous said...

Who are you Lulu? Au unatafuta kiki? Na kwa kipi hasa ulicho nacho? Wabongo achene sifa za kijinga

Anonymous said...

Safi sana lulu nakukubali we ni mzuri bwana, usikubali kuchezewa na diamond kwani wewe huyo siyo type yako. Endelea kujenga heshima yako wewe siyo papa la mji.

Anonymous said...

Wewe mtoto tulia kabisa na umwonbe mungu azidi kukupingania kwa yaliyopita na marehemu K. Achana na ya dunia mrudie Mungu hujajifunza tu

Anonymous said...

Lulu ulisema umeokoka, kama ni kweli simama kweli kweli. Mungu amekusamehe kwa kuhusika na kifo cha K. Achana na midhambi ya dunia. Hao au huyo msanii ni wakala wa shetani kwa 100% Mwogope sana Mungu

Anonymous said...

I love u Lulu...thanx for standing up to this clown who thinks women are disposable underwear. And for you Wema na Penny...esp. Wema why stoop so low...u act so desparate. He should be desparate to have you n not vice versa . Penny hela yake ndogo matbe ndo maana anatake shit from Diamond ila wengine hataa. So proud of you Lulu. I wanna adopt you as a lil sis.

Anonymous said...

Wee fala hapo juu acha majungu, toto la kichaga liko bomba , lulu mdogo wangu uzi huo huo usikubali kuchezewa na mafala kama kina diamond, jitahidi kula jasho lako na mungu atakusaidia, WANAWAKE JUUUU

Anonymous said...

Kwanza kabisa dunia imekuweka katika jopo la wasaliti sasa unachojipigia debe ni nini mwanangu fanya taratibu huhitaji kujieleza.

Anonymous said...

Huyo anayejiita diamond ni wakala wa shetan, kweli katumwa kuja kuangamiza wanawake. Kweli kuna siku watu watakaa chini waanze kulia bila msaada wowote. Mwisho wa vitendo vyake uu karibu sana. Tena nahisi mchawi, au anasaidiwa na waganga. Lulu jitahidi uachane naye mwaya mdogo wangu, tena hata usimsogelee kabisa asije akakupakaza ushenzi wake huo

Anonymous said...

We Mtoto Cute Lulu tulia muombe Mungu wako fanya kazi zako za Kisanii Hayo mabalaa mengine unayotaka kuanza hayafai tulia Dogo piga kazi uongeze kipato nenda hata shule zaidi ya mambo ya Filamu au Sanaa mungu anakupenda achana na hayo mabalaa ya wanaume ndio wewe ni mzuri tunza heshima yako GODBless

Anonymous said...

huna jipya kwa uzuri gani ulionao? au kwavile unachukuliwa na wabunge acha nyodo na kujiona wewe ni bab kubwa huna jipya na hayo uanayoanzisha haya sera yoyote

Anonymous said...

nyie wote mnamuunga mkono huyo lulu mnashangaza sana kwani huyo diamond anawabaka hao wanawake au wanajipeleka wenyewe? kuweni wabunfu wa mambo mengine acheni majungu huyo lulu ana kipi cha ajabu? badirikeni fanyeni kazi acheni majungu wangapi tunawaona au kwavile hawaandikwi?

Anonymous said...

Mwambie kama anakupenda akuoe kabisa atoe mahar kwanza ndoa ifungwe ndipo mambo mengine yaendelee coz nikicheche