Advertisements

Saturday, December 7, 2013

TANZANIA UHURU NIGHT WASHINGTON, DC, MHE. JANUARY MAKAMBA KUWA MGENI RASMI

 ITAKUWA SHEREHE YA KIHISTORIA
 Hatutauza tkt mlangoni, TIKETI ZOTE 
Kwa maelezo zaidi piga simu kwa Dj Luke 301 661 6696,  Dj Seif  202 286 6595 na Baraka Daudi 301 792 8562 

TANZANIA UHURU NIGHT Itaanza saa 12 jioni (6pm) kwa COCKTAIL tafadhali wahi mapema ule na faida ukichelewa utapata hasara.
Hawa ndio watakaopendezesha Uhuru  Bar
Kristina                             Sonia                                        Nina
Uhuru Red Carpet

VIJIMAMBO Blog inakuletea TANZANIA UHURU NIGHT siku ya Jumamosi December 7, 2013 Ukumbi wa THE FRIENDSHIP CENTER, 9055C Maier road, Laurel, MD 20723 na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mhe. January Makamba kuwa mgeni rasmi
Ni usiku wa Uhuru wa Tanzania, kula, kunywa mpaka unasaza kwa $60 tu na muziki ni mpaka asubuhi nunua tiketi yako mapema nafasi za kukaa ni watu 200 tu na 
Mimi ni mtanzania, natoka Tanzania, nchi yangu Tanzania, MIAKA 52 ya UHURU wa TANZANIA.

ALL YOU CAN EAT AND DRINK ALL NIGHT FOR $60 ONLY

DRESS TO IMPRESS NO JEANS, SNEAKERS, SANDALS OR T-SHIRTS

WATOTO HAWARUHUSIWI


KARIBUNI WOTE

43 comments:

Anonymous said...

Too expensive.

Anonymous said...

Uncle ungefanya hata $30 ..$60 hutupati...hatuitaji chakula wala vinywaji.. Weka music tuu.

Anonymous said...

Waheshimiwa hili ni swala zuri sana mliloamua kufanya hapa dc but mbona kuna mapungufu kidogo kama mke na mume itakuwa kiasi gani? Hamuoni kama hiyo amount ni kubwa sana? Je ni aina gani ya menu itakayokuwepo na jinsi gani utanihakikishia kula mpaka kusaza. Maana shughuli nyingi zimepita na huu msemo umetumika but hatujaona ukweli. Please go back review then tupeni new price inayokubalika.

Thanks
Mdau

Anonymous said...

Kaka luke..kama dinner yenyewe ni farida catering kwa 60 dollar ! Samahani sana.. Usijiingize kwenye trend za ajabu utajiharibia jina.. Wewe unajulikana sana kama mwana jamii na unaheshimika. Weka kiingilio fair na chakula wanunue. Angalia watu waliofanya sherehe za madola 60 mpaka mia wako wapi? Hauwasikii hata mjini.. It is nt worth it.. Kutoka mdau wa vijimambo

Anonymous said...

Wadau wa vijimambo acheni kulalamika kwa $60.00. hebu tujaribu kuibreak down kwa mume na mke au couple kwa jumla ya $120.00. tutumie vigezo vya club; kiingilio kwa mtu mmoja ni $20.00(couple $40.00),classic dinner plate per person$25.00(couple $50.00),three drink any liquor/wine/beer $15.00(couple $30.00). kwa wadau wa vijimambo utaona tayari umepata mahesabu yako kamili. tunataka vitu classic kwa watu classic tukienda mahali tuenjoy event,na vijimambo wameshatuonyesha kwa miaka mitatu kila wakitufanyia party inakuwa babu kubwa. tunaamini na hii itakuwa babu kubwa,vijimambo hawana usanii. tena bro' Luke nafikiri ingekuwa dola mia moja ili iwe more classic. tuletee vitu kaka.

Die hard fan wa vijimambo said...

Mdau hapo juu sikatai vijimambo inatupaga vitu classic ila upande wa menu huwa anatuangusha kila siku..kama ulivyosema sahani mtu dola 25 but kinakuwaga mlo wa maana silipi 25 kwafarida catering.. 60 kwenye centre!! No way .. Kaka luke wanataka kukulostisha hawa jamaa achana nao.. Fanya mambo ya kawai4ya vijithings tuburudike.. Kwa 60 mtajikuta wewe baraka na dj seif ,na wachache wasimamizi wako. Sisi wengine utatusamehe

Anonymous said...

Muda uliopanga ni mapema sana. Wengine tunakuwa hatujatoka makazini.

Anonymous said...

Acheni mambo ya kishwahili kulalamika bila mpango kwani mmelazimishwa kwenda hiyo ni biashara watu wanataka kutengeneza faida ..dj luke anawalisha na kuwanywesha bure takribani miaka3 party ya vijimambo!!mbona watanzania mnapenda kulalamika!!if u can afford kaa nyumbani!!

Anonymous said...

Dezo dezo, Ndalla Kasheba aliimba. Wote wanaolalama mnaonaje kweli wandugu Luke amekuwa anawalisha na kuwanywesha sana leo iweje? Jipangeni vizuri bado mapema sana wajemeni. Decembar bado mwezi mmoja mkubwatoka sasa.

Anonymous said...

Anza kusevu dola 5 kila wiki kuanzia sasa utapata hizo hela.

Anonymous said...

$60 mbona ndogo sana

ukiigawa hivi
$20 - kiingilio
$20 - msosi (bei ya kawaida tu)
$20 - vinywaji (kwa wale wanywa bea hapo ni bia 4 tu, lakini hapo unapata unlimited)

ila ma-caterers wa DVM jaribuni ku-improve quality ya vyakula vyenu maana siku hizi mmeanza kulipua lipua



Anonymous said...

Mbona price nyingine tena kwenye hiyo online clink yenu $62.49 . Please wekeni vitu wazi tuu. $60 au 62.49 ( transparencies point )

Anonymous said...

mdau hiyo ya online(pay pal) kuna tax ya $2.49,ndio maana take advantage ununue kwa kila dj Luke ili usilipe tax.

Stake holder said...

Maoni ni sehemu ya kufanikisha na si malumbano, hivyo ni juu ya kamati ya maandalizi kuyaangalia kwa mtazamo mzuri, bado naamini kuwa $60 ni kiwango, nadhani chakula na vinywaji vingeuzwa ili kutoa kwa kila mtu kuamua badala ya kuwa pre-paid, hii ni siku ya kitaifa hivyo ingelenga kuwajumuisha wadau kwa ajili ya kuifurahia na si kibiashara. Si wote tunaokunywa beer wala liquor na si wote watakaopenda kula. Iandaeni kwa namna ambayo itamuwezesha kila mtu kuhudhuria.

Anonymous said...

Hawa mabalozi wanakuja huku West kujishughulisha na hizi cooking events?

Kwa nini sijasikia huyu Balazi kutembelea state ambazo zinaongoza kwa uchimbaji wa Gesi na Mafuta ili aweze kuitangaza Tanzania?

Anonymous said...

mdau kuwa na heshima,labda hujui unachoiandika. umeshajaribu kumualika balozi kutembelea hizo state unazozingumzia au unaanza kulaumu tu bila kufanya utafiti. kaka luka na wewe acha kutupostia hizi post ambazo hazina maana yoyote zaidii ya kubomoa community yetu. hii ni siku ya kusherekea uhuru wa miaka 52 ya nchi yetu. kama wewe una uchungu na nchi yako njoo ushiriki na utapata muda wa kukutana na balozi na kumueleza ideas zako sio kukaa na kuanza kulalamika bila msingi.

Anonymous said...

Dj Luke,wengi tunataka kuja,naomba uwe flexible na rate,umesema cocktail ni 6 to 8 pm,kama mimi nakuja after 10,nimelipa $60,nitakunywa nini,na je dinner nayo inaisha saa ngapi? Kama nanunua drinks after 8,kwanini usiweke pay at entrance option with range of time ili iwe fair kwa wote. Anayekuja kula,kunywa bure na anaekuja late kulipia same rate for me it does not make sense!!just sayin!

Anonymous said...

kama haimake sense kaa nyumbani si lazima uwepo wewe. wabongo kila kukicha kukosoa ya wenzao, kama tumelogwa. sijui ni elimu, sijui ni utamaduni . Luka anzisha ukurasa wa kufundisha tabia wazee wastaarabu wajaribu kuokoa jahazi.

Anonymous said...

Wajasirimali wabongo mna jeuri halafu mnakuja ku beg hela zetu,mtu anauliza kiungwana kuhusu options za rate & time,unajibu kama ngumbaro,halafu mwataka kuwa wafanyabiashara,i suggest u go back to school for communication skills 101,. Kwa lugha zenu hizo mtahassle saaaana mpaka liamba

Anonymous said...

sikiliza we unayejiona msomi, ngoja nikupe shule sasa. Hebu nenda Verizon center useme naingia kipindi cha pili cha mechi ya wizard na niko tayari kusimama msinipe kiti ila niuzieni tiketi kwa bei nusu halafu uje hapa utuelimishe ilikuaje. Mtanzania kuandaa event haimaanishi hana gharama au haitaji faida. Fikra za kushusha bei ndizo zinafanya event za watanzani kufanyika kwenye vijisehemu chafu, hamna hewa, usalama ni usiku utata...nk. sasa siku hii watu tutapiga suti, na magauni ya siku kuu wee endelea kupiga vijembe wakati hata baiskeli huna na unalia njaa tangu uondoke tanganyika 1980. una dola ngapi benki kwa kusave kilaza we!

Anonymous said...

mie nashangaa, mtu kaandaa event watu wanataka kuibadilisha according to their shejo and preferences. utawaplease wangapi?

Anonymous said...

Lol wabongo mnavituko. Kama ni bei basi wacha shughuli ikupite mi sioni kwanini mnalumbana. Mdau UK

Anonymous said...

Hamna tatizo,mimi nafanya party ya Uhuru bure,njooni,mnywe,mle na to go,bureeee!! Tega sikio for venue,date dec. 7@10pm,air ticket on u,,zingatia muda tafadhali,


Mdau bongo,Tz,teh!teh!

Anonymous said...

Wadau kama huwezi kwenda na huna mfuko mnene kalagha bhao. sisi tutaenda kuvuta raha zetu,wewe kaa kulumbana.

Anonymous said...

hii ni kama ile dinner iliyoandaliwa na tano ladies au ile white boat party, ni kwamba unatakiwa kuwepo mwanzo hadi mwisho wa event.

Anonymous said...

mdau acha zako,huwezi kucompare tano ladies au boat party na shughuli za vijimambo. always vijimambo wanatupa vitu free na sasa hivi wameamua a small fee I think will be the best of the best. hongera sana dj luke,dj seif na Baraka. tunakuja kusupport event maana tunajua itakuwa babu kubwa. tayari vijimambo imeshatuonyesha mfano,tuwekeeni vitu vya nguvu muwafunge midomo hao wenye mifuko midogo na wabwabwajaji.

Anonymous said...

Na wewe siufanye yako ya bure muulize vizuri Luke anavyo jishugulisha halafu wewe unasema bure umezowea dezo .twende kumuunga Luke mkono is vinginevyo maneno hayajengi.

Anonymous said...

MNABISHANA KUHUSU BEI YA KULA HAMBISHANI TOKA TUPATE HUU UHURU TUNAENDA WAPI TUNAELEKEA WAPI TAIFA LETU LIMETULETEA NINI NA SISI TUMELILETEA NINI KAZI KUJISIFU TU KWA KULA NA KUVAA NA MISTAREHE YA KIPUUZI BADALA YA KUPANGA MAISHA YENU NA KUJUA HUU UHURU UNAMAANA GANI KWETU WATANZANIA NDO MAANA KILA SIKU TUNAKUWA WATU WA BURURUZWA KAMA TAKA TAKA ZA MITAANI NA KUTIWA KATIKA GARBAGE TRUCK TURUSHWA DAMPO

AKILI FINGU WENZENU HUWA WANA DISCUSE ISSUE ZA MAANA YA UHURU WENU NYI MIPOMBE NA MIVYAKULA NA MISTAREHE YA KIPUUZI NA KUOTA VITAMBI UTAFIKIR VIPAKACHA VYA DAGAAA WA FERI

POLENI WADANGANYIKA WENZANGU POLENI SANA

LUKE BIG UP MAN YOU DO YOU THING WAJINGA NDO WALIOWAO SIKU ZOTE BIG UP MAN YOU ARE GREAT THE GREATEST

Anonymous said...

tumeka na kujiuliza baada ya starehe hizi nini maana ya uhuru wa nchi yetu na faida zake na hasara zake kwa wananchi wote hasa hasa wa vijijini waliopo nyumbani.

au basi tunasherehekea tu bila kutafakari huu uhuru wetu na kizazi chetu.

tukuwe watanzania tuwe watu wa kufikiri na kuona mbali sio wafikiriwa

shukran

Anonymous said...

Uhuru wa tanzania.. Kutoka kwa nani.. Mbona mnadanganya umma.. Hamna kitu uhuru wa tanzania.. Hiyo mnayosheherekea ni tanganyika ....acha kujidanganya..

Anonymous said...

msije msije vishoka vya kupiga maboksi kaeni pigeni maboksi halafu muende job inginewe tena mpige maboksi ndo mlichokijia marekani pigeni maboksi yenu wee mpake mtoke roho zenu na kuzeeka bila mpango msije kwenye uhuru wetu wacha tuserebuke wenyewe kwanza wabahili wakubwa wakutoa pesa zenu mtakufa nazo hizo mnatuchafua bwana na wewe luke usiweka comment za hawa wachovu wapiga maboksi hawajui starehe zaidi ya kwenda makazini kupiga maboksi na njaa zao

ohaa njoeni wangwana wenye kumudu kulipa kiingilio mpate burudani poa wasio taka waende wakapige maboksi na ubahili wao na watoke roho zao

Anonymous said...

dj luke,dj seif na Baraka naombeni mniwekeeni tiketi kumi mimi na washikaji tunakuja hawa vimwana si mchezo. duuuh afadhali tumechoka na kuwa na bartender wanaume. mambo ya vijimambo kweli mazito. manshalaah nabata ushungu sasa. jamani msimalize tiketi tuje.

Anonymous said...

Duh Luke kumbe $60 imekuwa inshu hivi watu mnanunua nguo bei ghali na mavitu yasiyo natija mnajibana mnalala njaa kwa ajili ya kuvitimiza lakini kumsaidia mtu mnakuwa wagumu kiasi hicho??? Kila mtu anawaza anatuibia sijui nini roho zetu mbaya ndio zinarudisha nyuma hata maendeleo ya nchi yetu.

Anonymous said...

Wengine sisi ni wazanzibari uhuru wa tanganyika hautuhusu... Badala ya kufanya sherehe za muungano tusherekee wote maana hiyo ndio sherehe ya watanzania.. Uhuru huu znz haijatimiza bado.. Na mkitangaza andikeni tanganyika msiwe malimbukeni kama hamjasoma.. Kirefu cha tanzania ni TAN tanganyika ZAN zanzibar IA .. Sisi wazanzibari hii sherehe haituhusu..

Anonymous said...

eti kuna mtu anataka kuja kwenye party ya uhuru ili atafakari hahahahah! oh lord wa-TZ mwisho!

Anonymous said...

sasa kama wewe ni mzanzibari na unajua kabisa hii party haikuhusu kitakachokuleta kwenye hii party hasa ni nini?

Anonymous said...

Lol..wewe Mzanzibari speak for your self, Listen!! na mimi mzanzibari vile vile na nakwenda, usianze kuleta uzanzibari na uzanzibara kwanye haya mambo, ukiamua kuto kuja hayo yatakua maamuzi yako, dont speak on behalf ya wazanzibari, SAWA YAKHE!!

Anonymous said...

Walevi tu nyie wote..kwenyw pombe mbio mkiitwa vikaoni kusaidia nchi hamuoekani..hakuna inayomshinda dollar 60 wengine priorty zetuni tofauti

Anonymous said...

Sasa hapa breaking news ya nini!!!!

Anonymous said...

nimekukukubali this time .Makamba .

Anonymous said...

Mimi sina Tatizo saana na $60,00. Tatizo langu nikuona Dj Luke anakuwa mpiga debe wa ccm. Huyu waziri January....kaja kuleta nini hasa. Sema yeye yupo kwenye safari zake na anafanya kupitia.....na je anakuja kwa gharama za nani? Tunao viongozi wengi wa kitaifa hapa Washington Dc. Au ndo hizo $60,00

Anonymous said...

sasa dj luke,dj seif,baraka haya ndio mambo tunataka kusikia. classic party hakuna jeans bwana acha tuvunje kabati na madroo tutilie vitu vya kuimpress. sasa hii ndio party,vijimambo bwana kweli ni majamboziii makubwa. mambo ya redii kapetiiii, titititititi,hahahahahah.

Anonymous said...

Watanzania acheni ushamba...UHURU gani wa Mtanzania wakati unapangiwa nguo ya kuvaa..mzee mwinyi yupo hapa kwa gharama za Watanzania...waziri kivuli..naye yupo hapa pesa za wabeba magunia..wakati shule za mikoa yao hazina hata vyoo..aibu.....eti wanaomba kuwa ma Raisi kwani wanauchungu na nchi..kweli?