Maiti ni wawili wanawake na watatu wanaume kwa mujibu wa taarifa za sasa hivi kutoka kwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri Bw. Abdi Omar amesema usiku huu katika taarifa yake na waandishi wa habari huko Bandarini Malindi. Mkurugenzi anasema bado wataendelea kesho asubuhi kuwatafuta watu waliopotea baharini katika maeneo ya Nungwi.
Maiti wote wameletwa mjini kwa ajili ya kutambuliwa wapo katika hospitali ya Mnazi Mmoja baadae serikali itaanda utaratibu wa kawaida kwa maiti hizi kuzikwa kama ni kupewa jamaa zao.
Mkurugenzi Abdi aliwaambia waandishi wa habari kwamba Manahodha hao walipofika Nungwi kuna watu waliwauliza ikiwa kuna tatizo baada ya kuona boti yao inazunguka zunguka hapo hapo lakini walijibu kwamba hawana tatizo na wanaendelea na safari lakini pia wakaulizwa na KMKM iwapo wanahitaji msaada lakini walikataa na kusema hawana tatizo na wakaendelea na safari.
Mkurugenzi huyo amesema juhudi za serikali zilichukuliwa lakini alikubali kwamba wananchi ndio waliosaidia kwa kushirikiana na vyombo vya usalama kusaidia kuwatafuta waliopotea.
Anasema jumla ya abiria 396 walisafiri na chombo hicho huku watoto wakiwa ni 60 lakini baada ya kufanya hesabu wakakuta idadi hiyo imepunguwa kuna watu kama 20 wamekosekana ndani ya chombo hicho na ndipo walipolazimika kufanya uchunguzi na kufuatilia huko Nungwi na kweli wamepata miili mitano na waliookolewa wakiwa hai ni watatu.
Kempteni Nassor Abubakar Khamis ameshikiliwa na jeshi la polisi kwa mahojiano.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi anasema baada ya kupata hizo taarifa waliwahoji wahusika wa boti lakini Manahodha wa boti hiyo alisema hajaona kama kuna watu wamepotea lakini wao waliona mizigo tu imeanguka.
Mkurugenzi huyo amesema juhudi za serikali zilichukuliwa lakini alikubali kwamba wananchi ndio waliosaidia kwa kushirikiana na vyombo vya usalama kusaidia kuwatafuta waliopotea.
Mkurugenzi Abdi anasema kwa kufichwa taarifa hizi kumesbabisha matatizo na kiukweli wangepewa taarifa mapema na Manahodha basi wangeweza kuchukua juhudi za haraka kufanikisha uokozi huo lakini wamepata taarifa kutoka kwa wananchi na sio kwa wahusika wa boti hiyo.
![]() |
| Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri Baharini. Abdi Omar Maalim akizungumza na waandishi wa habari huko Malindi Zanzibar. |

No comments:
Post a Comment