ANGALIA LIVE NEWS

Saturday, February 22, 2014

HII NDO STORI YA MWALIMU ALIYEUAWA BAADA YA KUMCHINJA MWANAFUNZI WAKE...


Mwalimu wa madrasa ya Ali Munawar, ustaadhi Mohamed Ngulanjwa (36) wa Mbagala Mianzini jijini Dar es Salaam, ameuawa baada ya kumchinja mwanafunzi wake.


Ustaadhi huyo aliyekuwa mwalimu wa madrasa na shule ya awali ya Ali Munawar, alimchinja mwanafunzi huyo jana saa 12.10 jioni kwenye eneo la madrasa baada ya kutenganisha kichwa na kiwiliwili
(hudugu)

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Temeke, Jonathan Shana, akizungumzia mauaji hayo , alisema tukio hilo la kinyama, lilishuhudiwa na wananchi waliomuua ustadhi huyo.
Alisema baada ya mwalimu kumuua mwanafunzi wake wa kiume alichukua kisu alichotumia pamoja na msahafu na kukimbia.
"Ilidaiwa kuwa alimchukua mtoto huyo , kumlaza chini kisha kumchinja kwa kutenganisha kichwa na kiwiliwili na kutelekeza vipande vya mwili wake kwenye varanda," alisema Kamanda Shana.
Baada ya mauaji hayo mtuhumiwa alianza kukimbia lakini wananchi walimvamia na kumshambulia kwa mawe na kila silaha iliyokuwa karibu na kumuua papo hapo.

Shana alieleza kuwa polisi walifika eneo la tukio na kuchukua maiti hizo na kuzipeleka hospitali ya Temeke.
Hata hivyo alisema jina la mtoto huyo mwenye umri kati ya miaka 10- 12 halikufahamika na polisi inaendelea na uchunguzi

3 comments:

Anonymous said...

Sasa Mh DJ Luke, hizi picha zinauhusiano gani na habari hii. Aliyechinjwa alikufa na aliyechinja alikufa. Polisi walifika kuchukua maiti zote mbili. Huyu anayechukuliwa na polisi sidhani kuwa ni maiti. Je ni huyohuyo anayelia hapo kwenye picha ya pili?

Anonymous said...

Nimeshindwa kupata uhusian wa picha na tukio la mauaji. Je huyu anaeonekana ktk picha ni mzazi wa mtoto aliyeuawa?

Tukio hili linasikitisha sana . Poleni wafiwa wa pande zote mbili.

Anonymous said...

Picha hii ni mnaigeria kamuua mkewe na yeye kahukumiwa kifo, Dj Luke usichanganye mambo sio lazima uweke picha.