ANGALIA LIVE NEWS

Thursday, March 20, 2014

Rais KIkwete akiandaa hotuba yake ndegeni kuelekea Dodoma

Kweli Urais hauna ubia wala muda ama sehemu ya kuchapa kazi. Wakati wowote na mahali popote ni sehemu ya kazi, kama inavyoonekana hapa ambako Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametulia ndani ya ndege akisafiri kutoka Dar es salaam kuelekea Dodoma huku akiifanyia kazi hotuba yake ambayo ataitoa katika Kikao cha Bunge Maalum la Katiba, Ijumaa, Machi 21, 2014.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amealikwa kuwa mgeni rasmi na kuhutubia Bunge Maalum la Katiba kwa mujibu wa Kanuni 7(1)g na Kanuni 75(1) la ya Kanuni za Bunge Maalum.

PICHA NA IKULU

5 comments:

Anonymous said...

Nilitegemea ndege hii ya gharama kubwa ingekuwa inayo meza ya maana si vikabati kama night stand. Angalia sasa rais anaandikia kwenye goti! Tungeweza ku-customize ndege wakati tulivyiwapa order ya kutengeneza hiyo ndege la sivyo rais ataendelea kuumia shingo na mgongo kwa kuinama.

Anonymous said...

Mungano mwisho chumbe kaeni na Tanganyika yenu.

Anonymous said...

Air Force One. Lol

AFRICA said...

Meza ya mbao ni hatari.Ajali ndogo itakua balaa.Usalama kwanza.

Anonymous said...

Meza ya mbao ni hatari.Ajali ndogo inaweza kuwa balaa.