Uchunguzi wa kipindi cha BBC Panorama unafichua
kuwa kampuni ya madawa Uingereza GlaxoSmithKline inakabiliwa na
uchunguzi wa kihalifu nchini Poland kwa kutuhumiwa kuwahonga madaktari.
Madaktari kumi na moja na mkurugenzi wa tawi la kampuni hiyo wameshtakiwa kwa rushwa kati ya mwaka 2010 na 2012.
Afisa mmoja anayehusika na uuzaji wa dawa za
kampuni hiyo amesema madaktari walilipwa kushinikiza mauzo ya dawa ya
pumu Seretide ya kampuni hiyo ya GSK.
Kwa upande wake GSK inasema imemuadhibu mfanyakazi mmoja na inatoa ushirikiano katika uchunguzi unaoendelea.
Iwapo tuhuma hizo zitathibitishwa, huenda GSK
imekiuka sheria inayopinga rushwa Uingereza na sheria ya Marekani
inayoharamisha rushwa katika nchi za nje. Ni haramu kwa kampuni zilizopo
nchini kuwahonga wafanyakazi wa serikali katika nchi za nje.
Daktari mmoja amekiri kufanya makosa, na
ametozwa faini na
amecheleweshwa kifungo. Alikiri kupokea pauni 100
kutokana na shinikizo la mwakilishi wa GSK, kwa malipo ya uhamasisho
kuhusu dawa hizo ambao hakuutoa.
Akosolewa na Kuadhibiwa
GSK imegundua utovu wa mawasiliano uliotekelezwa
na mfanyakazi mmoja ambao ni kinyume na sera za kampuni hiyo katika
mafunzo ya kuimarisha viwango vya utafiti na mafunzo ya kiafya kuhusu
magonjwa ya kupumua yaliotoloewa na madaktari kati ya mwaka 2010 hadi
2012.
GSK ilifanya uchunguzi wa ndani na nje ya
kampuni hiyo baada ya kupokea tuhuma kadhaa kuhusu jinsi mafunzo hayo
yanavyotolewa katika eneo la Lodz.
GSK inasema: "Tunaendelea kuchunguza haya mambo na tunashirikiana kikamilifu na CBA". Ofisi kuu nchini Poland inayokabiliana na rushwa.
Mnamo 2012, GSK ililipa $ bilioni 3bn (£ bilioni
1.9) I katika kesi kbwa ya udanganyifu katika sekta ya afya katika
historia ya Marekani, baada ya kukiri makosa ya kuuza dawa mbili kwa
matumizi ambayo hayajaidhinishwa na kutoripoti kuhusu usalama wa kutumia
dawa ya kisukari kwa taasisi ya vyakula na madawa nchini
BBC
No comments:
Post a Comment