Advertisements

Wednesday, April 16, 2014

SERENGETI: KUNDI LA TEMBO LAVAMIA MAKAZI YA WATU NA KULA MAZAO YALIYOKUWA MASHAMBANI NA VYAKULA WALIVYOHIFADHI




KUNDI kubwa la Tembo zaidi ya 40 kutoka katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti wamevamia katika makazi ya watu na kufanya uharibifu mkubwa wa mazao pamoja na vyakula vilivyokuwa vimehifadhiwa katika kijiji cha Mwachumu kata ya Girya Wilayani Bariadi mkoani Simiyu.

Diwani wa kata ya Girya Safari Lewa alisema kuwa tukio hilo limetokea juzi majira ya saa 10:00 jioni katika kijiji hicho ambapo tembo hao waliingia kwenye makazi ya watu na kufanya uharibifu mkubwa wa mazao mbalimbali yakiwemo Mahindi pamojana na Pamba katika mashamba ya wananchi.

Lewa alisema kuwa zaidi ya hekari 60 za mazao ya Mahindi na Pamba zimeharibiwa vibaya na tembo hao na kwamba kwa sasa wananchi wa kijiji hicho wanaishi kwa wasiwasi mkubwa wakihofia kushambuliwa na tembo hao.

Alibainisha kuwa kutokana na wananchi hao kushambuliwa kwa mazao yao na tembo pia watakabiliwa na upungufu wa chakula na ameuomba uongozi wa hifadhi hiyo kuwasaidia wananchi waliodhulika na tembo hao kuwaletea chakula pamoja na kuja kuwatoa tembo hao katika maeneo ya makazi ya watu.

‘’Tuwe na usawa kwa wote pale wananchi waingizapo ng’ombe katika eneo la hifadhi hutozwa faini kali pia na wao wanapaswa kutoa fidia kwa wananchi wetu ambao wanaharibiwa mazao na wanyama’’alisema Lewa.

Mmoja wa wananchi hao kutoka kijiji hicho Mhoja Jilinge alisema kuwa tembo hao walivamia jioni mashamba yao ikiwa mazao bado hawajavuna na kuanza kushambulia hali ambayo inaonyesha kuwa hifadhi hiyo imekosa uangalizi mzuri pia hofu iliyopo kumaliza mazao na kudhuru watu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Bariadi Abdallah alikiri wanyama hao kuvamia maeneo hayo ambapo aliwaomba wananchi na viongozi wa maeneo hayo ambako tembo wamevamia wawe wanatoa taarifa mapema ili hatua za kuwarudisha hifadhini ziweze kuchukuliwa haraka.

Imechapishwa na kareny sungwa

No comments: