TAARIFA KWA UMMA
Naibu
Waziri wa Fedha(S) Mh:Mwigulu Lameck Nchemba(Mb) na Naibu Katibu Mkuu
wa CCM-Tanzania Bara ataongoza Sherehe za Kuadhimisha Miaka 50 ya
Muungano wa Tanzania Kwa Watanzania Waishio Nchini
Marekani-Washington-DC na Viunga Vyake.
Maadhimisho hayo yanayotegemewa Kufanyika Tar.26/04/2014 katika Ukumbi wa MATINICE EVENTS AND CONFERENCE CENTRE,7925 CENTRAL AVE,CAPITOL HEIGHTS,MD 20743.
Mh:Mwigulu
Nchemba aliyealikwa na
Balozi wa Tanzania Nchini Marekani Mh:Libereta
Mulamula kuongoza Sherehe hizo za Maadhimisho ya Miaka 50 ya
Muungano,atazungumza na Watanzania kuhusu Muungano
Wetu,Kuulinda,Kuutetea na Kuudumisha kwa Manufaa ya Taifa letu la
Tanzania na Watu Wake.
Watanzania Wote Mnaombwa Kufika kwa Wingi kwenye Maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhai wa Muungano Wetu,Hii ni nafasi nzuri kwa Watanzania Nchini Marekani kuandika Historia Mpya kwa Taifa letu.
Mungu Ubariki Muungano Wa Tanzania,
Mungu Ibariki Tanzania.
Imetolewa na
Ofisi ya Naibu Waziri wa Fedha(S)
Mawasiliano.
23/04/2014
1 comment:
hapa serikali ni tatu ili tuone vita ya lukuvu
Post a Comment