ANGALIA LIVE NEWS

Monday, May 19, 2014

KWA TAARIFA YAKO: USHIRIKINA WA MAMA WA KAMBO CHANZO CHA SOLOMON MUKUBWA KUKATWA MKONO

Haya msomaji wetu wa Gospel Kitaa karibu katika kipengele chetu cha ''KWA TAARIFA YAKO'' ambacho kinakujia kila siku za alhamisi ndani ya GK kikiwa na lengo la kukupatia habari ambayo iliwahi kutukia lakini yawezekana huijui pia yawezekana ilitukia ukawa unaijua lakini GK ikawa imesahau mahali au kuna sehemu haina usahihi utapata fursa ya kusahihisha kwa kuweka comment yako chini kabisa kwenye habari husika. Karibu
Solomon Mukubwa akiwa katika pozi na mtangazaji wa Wapo Radio Fm Silas Mbise.          
Hii leo KWA TAARIFA YAKO kama hujui ni kwamba mwimbaji nyota wa muziki wa gospel Afrika Mashariki mwenye asili ya Kongo bwana Solomon Mukubwa ambaye ametamba sana na kibao chake cha ''Mfalme wa Amani'',  ana ulemavu wa mkono wa kushoto baada ya kukatwa akiwa mtoto mdogo, ukweli ni kwamba mwimbaji huyo alizaliwa akiwa mzima bila ulemavu huo wa mkono, katika mazungumzo ammbayo amewahi kufanya na Wapo Radio Fm kupitia kipindi cha gospel celebration kinachoongozwa na Silas Mbise, Mukubwa allitabanaisha kwamba kilichosababisha kukatwa kwa mkonoo wake ilikuwa sababu za kishirikina zilizosababishwa na mama yake wa kambo kwakuwa baba yake alikuwa na wake wawili (kama nakumbuka vyema).
Mukubwa amesema mama huyo alimrushia mapepo yaliyosababisha mkono wake kuanza kuoza kila iitwapo leo hadi kufikia hatua ya kuambiwa hospitalini kwamba inatakiwa mkono huo kukatwa kama anahitaji kuendelea kuishi hali iliyolazimu akubaliane na uamuzi huo wa madaktari hivyo  mkono wake mmoja kukatwa baadaye Solomon aliokoka na kumjua Mungu hivyo kujikita katika imani yake ya kumwamini Mungu ambapo mama yake huyo naye alipata kilema cha macho ( kama nakumbuka vyema) Pia mama yake huyo alikiri kuwa ndiye aliyehusika na ulemavu huo wa mkono wa Solomon.

Hata hivyo pamoja na hayo yote Solomon Mukubwa alimsamehe mama yake huyo pia huwa hapendi kuzungumzia kisa hicho zaidi anataka kumtangaza Kristo, kisa hiki ni kirefu na mengi nimeyaacha kama unayakumbuka endelea kwa kukomenti chini ya habari hii. Pia GK inatarajia kumtafuta Mukubwa ili ipate kisa kamili.

No comments: