Advertisements

Saturday, May 24, 2014

SIKU YA FISTULA DUNIANI YAADHIMISHWA ZANZIBAR‏

Mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya siku ya Fistula, Mwakilishi wa Baraza la wawakilishi, Wanu Ameir (kushoto) akipokewa na Balozi wa Fistula, Khadija Salum baada ya kuwasili kwenye hospitali ya Kwamtipura mjini Zanzibar jana,wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Fistula Duniani na utoaji wa elimu kwa Umma kuhusu tatizo hilo.Elimu hiyo ilitolewa kwa ushirikiano wa wadau wa CCBRT,UNFP,Vodacom Foundation.
Wananchi wakimsikiliza mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya siku ya Fistula Duniani na utoaji wa elimu kwa Umma kuhusu tatizo hilo.Elimu hiyo ilitolewa kwa ushirikiano wa wadau wa CCBRT,UNFP,Vodacom Foundation. .
Mgeni rasmi, Mwakilishi wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Wanu Ameir akizungumza kwenye hafla ya siku ya Fistula kwenye hospitali ya Kamtipura mjini Zanzibar jana.katika siku hiyo maalumu Duniani na utoaji wa elimu kwa Umma kuhusu tatizo hilo.Elimu hiyo ilitolewa kwa ushirikiano wa wadau wa CCBRT,UNFP,Vodacom Foundation.
Mgeni rasmi na viongozi wengine wakiomba dua baada ya hafla hiyo ya siku ya Fistula Duniani jana,ambapo alitoa mada na elimu kwa Umma kuhusina na tatizo hilo linalowakabili wakina mama.Elimu hiyo ilitolewa kwa ushirikiano wa wadau wa CCBRT,UNFP,Vodacom Foundation.

Mwakilishi wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar(viti maalumu), Wanu Ameir, amewataka viongozi wa mikoa ya Zanzibar kutoa mazingira wezeshi kuwarahisishia mabalozi wa Fistula nchini kuhamasisha na kuelimisha Umma dhidi ya fistula hapa visiwani,

ambapo mpaka sasa ni wagonjwa 6 tu ambao wamejitokeza tangu kuanza kampeni hiyo aliyasema hayo wakati wa maadhimisho ya siku ya Fistula Duniani jana.Elimu hiyo inatolewa kwa ushirikiano wa wadau wa CCBRT,UNFP,Vodacom Foundation.

1 comment:

Anonymous said...

ccm nzuri sana kwa kuwapenyeza okoo wao akiwa mama madarakani anachukua mwana akiwa baba madarakani naye mama anachukua ndo maana hawataki serikali tatu itakayo wajibisha na kuwa na nidhamu na uwajibikaji si kuchomekeza familia zao kama kampuni ya mtu binafsi.

ccm oyeee oyeee oyeeeeeee kwa kuchomekezana familia zao ndani ya chama chao